• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAZIRI WA TAMISEMI SULEMANI JAFO AZINDUA MFUMO WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA, AKEMEA SUALA LA UTUMIAJI WA FEDHA MBICHI. GEOGRAPHICAL

Posted on: March 15th, 2019

Na mwandishi wetu.

Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jafo jana march 14 katika ukumbi wa NSSF uliopo manispaa ya Kigoma/Ujiji alizindua mfumo wa taarifa za kijiografia (GIS) uliofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa kimkakati wa ukuzaji wa miji na majiji Tanzania(TSCP).

Akihutubia katika ukumbi huo alisema mfumo huo utasaidia katika ukuzaji wa mapato kwa halmashauri na namna ya kuwahudumia wananchi waliopo katika Manispaa hiyo kutokana na mfumo huo kuwa na taarifa mbalimbali zitakazoanza kukusanya kutoka kwa makazi yote, biashara na huduma za jamii zilizopo katika eneo husika.

Alisema Manispaa ya Kigoma/Ujiji ndio imekuwa sehemu ya kuandalia mfumo huo ikiwa imepangwa kutumika katika halmashauri nane zinazopitiwa na mradi wa TSCP na kufadhiliwa na Benki ya Dunia huku akiwataka watendaji kujifunza Mfumo huo na kuhakikisha wataalamu wa Tehama waliopo katika halmashauri zote nane wanatoa ushirikiano katika mfumo huo.

Akiendelea kuhutubia aligusia suala la upotevu wa mapato kutokana na upotevu wa mashine za kukusanyia mapato(POS) huku akiasa halmashauri kuchukua hatua za kimaadili katika upotevu huo huku akiasa halmashauri katika tumiaji wa fedha mbichi ambazo zinakuwa hazijafata taratibu katika kufikia matumizi.

Naye Eng.Mussa Nati mhandisi na mtaalamu wa mfumo wa GIS kutoka Benki ya Dunia alisema mfumo huo tayari umeshaanza kutumika katika wilaya ya Kinondoni na umeleta tija katika ujenzi wa barabara namna ambavyo haikuwa tatizo la migogoro ya fidia kwa wakazi huku akieleza umeweza kukuza mapato katika wilaya hiyo huku akitoa rai mfumo huo kutumika vizuri na kuulinda kupitia wataalamu waliopo.

Naye meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Hussein Ruhava alishukuru kwa kuona uzinduzi huo kufanyika katika manispaa hiyo huku akisema ni heshima kubwa ambayo serikali imeitoa huku akiahidi kutoa ushirikiano na madiwani wote katika ukusanyaji wa mapato kutokana na mfumo huo na kuitaka serikali kuitazama zaidi manispaa hiyo kutokana na uwepo wa huduma duni zilizopo.

Naye mkuu wa wilaya ya Kigoma kwa niaba ya Mkuu wa mkoa Ndugu. Akitoa salamu kutokana na mfumo huo alisema kupitia ofisi ya Mkuu wa mkoa itatoa ushirikiano kwa kusimamia na kuhimiza halmashuri kutumia mfumo huo kwa usahihi na bila kuingilia mfumo huo katika uhalifu.

Waziri huyo baada ya kumaliza mkutano huo katika ukumbi wa NSSF ambapo viongozi mbalimbali walihudhulia kutoka ofsi ya Mkuu wa mkoa, Wakuu wa wilaya zote za mkoani Kigoma, wakurugenzi wa Halmashauri, Meya wa manispaa ya Kigoma/Ujiji, Mkurugenzi wa Kigoma/Ujiji, Madiwani, wataalamu, wenyeviti wa mtaa pamoja na waandishi wa habari alifanya ziara katika eneo la Msimba lilopo dampo la taka la manispaa hiyo ambapo alitoa tamko kuanza kutumika kuanzia sasa.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa