• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

AHADI YA RAIS SAMIA UJENZI WA SOKO LA KIBIRIZI KISASA WAANZA KUTEKELEZWA. Market Construction

Posted on: October 27th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Ahadi  ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani juu ya ujenzi wa Soko la Kibirizi kisasa imeanza kutekelezwa  kwa Viongozi kuanza kutembelea na kujadili namna  ujenzi  huo utakavyotekelezwa  sambamba na Ujenzi wa barabara inayopita katika eneo hilo

Akizungumza katika kikao kilichofanyika Leo Oktoba 27, 2022  katika   Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhandisi kutoka Mamlaka ya Bandari (TPA) Makao makuu Eng. Twaha Msita amesema timu ya Wataalamu imekuja kwa lengo la kuangalia namna ujenzi wa soko hilo utakavyotekelezwa kama ilivyoahidiwa na Rais katika ziara yake aliyoifanya hivi karibuni Mkoani  Kigoma

Amesema katika ziara yao wametembelea  eneo  la soko la Kibirizi  ili  kupata ukubwa wa eneo, uchoraji ramani na kupata mapendekezo ya gharama ya ujenzi ikiwa ni hatua ya awali kwa lengo la kuboresha Mazingira ya Wafanyabiashara na Wajasiriamali wa Soko hilo

Ameendelea kusema kukamilka kwa ujenzi wa Soko hilo kisasa utawanufaisha  Wafanyabiashara walio wengi na biashara kufanyika katika nyakati zote ukilinganisha na sasa eneo hilo kujaa maji

Amesema miundombinu itakayojengwa katika Soko hilo ni pamoja na ujenzi wa Shedi za Wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi, Mabanda,  Ujenzi wa Migahawa ya vyakula, Ujenzi wa vituo vya kupaki daladala, Bajaji na boda boda

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Evans Mdee amesema Manispaa hiyo inazingatia maagizo yaliyotolewa na Rais kwa kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa Soko hilo   kabla ya kuanza kwa mradi  ili kuona namna watakavyoweza kupisha ujenzi huo

Amesema  Wafanyabiashara na Wajasiriamali  watakaopisha ujenzi huo watapewa kipaumbele pindi ujenzi utakapokuwa umekamilika

Amesema kuboreshwa kwa Soko hilo kwa ujenzi kisasa kutakuza Mapato ya Wafanyabiashara, kuvutia Wateja na Wafanyabiashara Wakubwa na kuongezeka kwa mapato ya Manispaa hiyo

Ahadi ya Ujenzi wa soko la Kibirizi Kisasa ilitolewa  na Rais October 18, 2022 wakati akihutubia Wananchi waliojitokeza kumpokea eneo la Kibirizi  mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika Ujenzi wa bandari  ndogo ya Kibirizi





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa