• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Miradi inayo Endelea

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ilipanga kutekeleza jumla ya miradi mitatu ya maji. Mradi wa maji wa Kibirizi (Group scheme), Mradi wa Maji wa Kagera na mradi wa Maji wa Mgumile.

Ujenzi wa Mradi wa Kagera (Buhanda na Businde) imeshakamilika na kukabidhiwa KUWASA kwa ajili ya kuunganishwa na bomba kuu litakaloingiza maji kwenye tenki


MRADI WA MAJI WA KIBIRIZI

Mradi huu umegharimu Tsh 325,095,920.00 (Mkataba wa awali kabla ya kusitishwa Tsh 1,092,945,590.00). Ulianza kujengwa tarehe 28.01.2013 na ulikuwa ukamilike tarehe 28.11.2013. Mkandarasi alikuwa D4N Co Ltd. – Kahama chini ya Usimamizi wa UWP Consulting Ltd – Dar es Salaam. Mradi ulikusudiwa kutoa huduma kwa watu 20,608 wa eneo la Kibirizi, Bushabani. Buronge na Mwasenga. 

 KAZI ZILIZOPANGWA KUFANYIKA KATIKA MRADI WA KIBIRIZI

Kujenga chanzo cha maji na kufunga pampu 2, Kujenga matenki 2 ya ujazo wa mita 225 (lita 225,000) na 135 (lita 135,000). Kujenga mtandao wa bomba wenye urefu wa kilometa 31. Kujenga magati 49 ya kuchotea maji. Kujenga nyumba ya mlinzi wa mitambo. Kujenga ofisi ya mradi.

KAZI ZILIZOFANYIKA

Ujenzi wa matenki ya ujazo wa mita 225 na 135 (Lita 225,000 & 135,000), ujenzi wa Magati ya maji 16 (hayajakamilika) kujenga mtandao wa bomba wa urefu wa kilometa 13. Ujenzi wa ofisi ya mradi ambayo imekamilika kwa 30%.



MRADI WA MAJI WA MGUMILE

Mkataba na mkandarasi wa ujenzi wa mradi huu ulisainiwa mwezi Aprili, 2014 lakini kukosekana kwa fedha  kulisababisha kusimama utekelezaji wake.

Hivi sasa fedha kiasi cha Tsh 549,828,345.00 zimepatikana toka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na utekelezaji wa mradi huu umeanza mwezi Februari, 2017.

Mradi huu utagharimu Tsh 549,828,345.00. Umeanza kujengwa tarehe 16.02.2017 na unatarajiwa kukamilika tarehe 30.07.2017. Mkandarasi ni Maginga Business Holdings Co Ltd. – Dodoma chini ya Usimamizi wa Mhandisi wa Maji wa Manispaa. Mradi umekusudiwa kutoa huduma kwa watu 2,795 wa Mtaa wa Mgumile.

 KAZI ZILIZOPANGWA KUFANYIKA KATIKA MRADI WA MGUMILE 

Kujenga chanzo cha maji na kufunga pampu 1, kuweka Solar panels, Kujenga tenki 1 la ujazo wa mita 80 (lita 80,000). Kujenga mtandao wa bomba wenye urefu wa kilometa 7.5. Kujenga magati 9 ya kuchotea maji. Kujenga nyumba  ya mitambo. Kujenga ofisi ya mradi.

 HALI HALISI YA SASA 

Kazi iliyokwishafanyika mpaka kufikia tarehe 17.03.2017, imefikia asilimia 5.5 ya kazi yote.

CHANGAMOTO ZILIZOPO KWENYE UTOAJI WA HUDUMA YA MAJI

Utekelezaji wa Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira na utoaji wa huduma ya maji unakabiliwa na changamoto zifuatazo;

Ukosefu wa miundombinu ya barabara kwa ajili ya kufikisha vifaa vya ujenzi kwenye eneo la mradi wa Mgumile kwani eneo hili kwa sehemu kubwa limezungukwa na Ziwa na Mto Luiche. Kujaa kwa Mto Luiche kunasababisha pia eneo la barabara pekee isipitike na hivyo kuchelewesha utekelezaji wa mradi.

Kuharibiwa kwa miundombinu iliyokamilika ujenzi wake katika mradi wa Kagera kabla ya kuanza kutoa huduma kutokana na kukaa muda mrefu.

Mamlaka ya Maji (KUWASA) kukosa fedha za kukamilisha ujenzi miradi iliyokabidhiwa kwao

  • Gharama kubwa za umeme (Wastani wa Tsh 100milioni kwa mwezi) kwa ajili ya kuendesha mitambo ya kusukuma maji
  • Uzalishaji wa maji ni mdogo kuliko mahitaji ya wakazi wa  Manispaa
  • Kuharibika kwa mitambo ya maji mara kwa mara kutokana na uchakavu
  • Mtandao wa mabomba uliopo una vipenyo vidogo, chakavu na haujaenea kwenye maeneo yote ya Manispaa.
  • Mamlaka ya maji kuwa na makusanyo madogo na ambayo hayakidhi mahitaji ya kulipa gharama zote za uendeshaji

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO

  • Mradi mpya unaoendelea kujengwa umeangalia kupunguzwa kwa gharama za umeme
  • Mamlaka ya Maji imefunga pampu mpya mnamo Januari 2017 ikiwa ni msaada wa kuboresha huduma ya maji kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji tukiwa tunasubiri kukamilika kwa mradi wa maji wa MDGI. Baada ya kufunga pampu mpya uzalishaji umepanda kutoka meta za ujazo 12,000 (Lita milioni 12) hadi 15,000 (lita milioni15) kwa siku. Migao ya maji imeongezeka kutoka mgao wa siku moja kwa wiki hadi siku mbili kwa wiki kwa masaa 9 kwa siku
  • Mamlaka inatekeleza Mradi mkubwa wa maji ambao hadi kufikia mwezi Machi 2017, utekelezaji wake umefikia asilimia 69. Mradi umechelewa kutokana na Mkandarasi kukosa fedha za kuendelea na mradi. Mradi ulipaswa kuisha Machi 2015.
  • Kufunga mfumo mpya wa kufanya malipo ya huduma za maji lengo likiwa kuboresha mapato na utoaji wa huduma kwa wateja kwa njia ya mitandao ya simu kama M-Pesa, Airtel Money, Tigopesa nk.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa