Na Mwandishi Wetu
Kamati ya Fedha na Uongozi Manispaa ya Kigoma/ Ujiji Leo Februari 18, 2026 imefanya ziara ya kutembelea miradi ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa.
Ziara hiyo imefanyika ikiongozwa na Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Musa Maulidi na Kuhudhuriwa na Wajumbe wa kamati hiyo(Waheshimiwa Madiwani) pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo.
Viongozi hao wamefanya ziara katika Ujenzi wa Soko la Kisasa katika Mwalo wa kibirizi unaendelea kwa gharama fedha za Kitanzania Billion Saba (Tsh 7,000,000,000/=) ukiwa katika hatua ya kujaza udongo na kuondoa maji.
Aidha Viongozi hao wametembelea na kukagua ujenzi wa ukumbi wa Kisasa unaojengwa eneo la Mwanga Community centre kwa gharama ya fedha za Kitanzania Billion 3.3/= hadi kukamilika fedha kutoka Mapato ya ndani ukiwa katika hatua ya Kupanga mawe na kutembelea ujenzi wa Shule mpya ya Msingi yenye Mkondo mmoja iliyopo Kata ya Kibirizi kwa gharama ya fedha za Kitanzania zaidi ya Million Mia mbili (Tsh 243,900,000/=) ukiwa umekamilika.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa