Ujenzi wa Soko la Mwanga Kisasa unaendelea kutekelezwa chini ya Mradi wa kuboresha Miji na Majiji kiushindani Nchini Tanzania (TACTICS) ukifadhiliwa na benki ya Dunia.
Tangu kuanza kwa ujenzi, Mradi umetoa ajira wakiwemo Wataalamu, Mafundi sanifu na Wasaidizi (vibarua) zaidi ya Elfu mbili Mia tatu (2300), wenyeji wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wakipewa kipaumbele.
Katika utekelezaji wa mradi Jamii imekuwa ikishirikishwa, na Wanaume zaidi ya Elfu moja mia sita (1,652) na Wanawake zaidi ya Mia Sita (648) wameendelea kunufaika na ajira mbalimbali katika Ujenzi huo.
Ujenzi wa Soko la Mwanga umeendelea kuwa na manufaa kwa Wajasiriamali kwa kuongeza kipato kutokana na ununuzi wa malighafi ikiwemo kokoto, mawe, mchanga na kuendelea kukuza uchumi wa Wakazi wa Manispaa hiyo.
Wanufaika Wengine ni pamoja na Wajasiriamali wa Chakula (Mama na Baba Lishe), Maafisa usafirishaji (Bodaboda) Wauzaji wa maji na wengine wengi.
Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kukamilika April 24, Mwaka huu na utaboresha miundo mbinu ya Wafanyabishara , kuvutia wawekezaji na kukuza uchumi wa Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa