Na Mwandishi Wetu
Wanafunzi wa kike katika shule za sekondari zilizopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji wamehamasishwa kupenda na kujiamini katika masomo ya sayansi ili kuweza kufikia ndoto zao.
Hamasa hiyo imefanyika Leo Februari 16, 2026 na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii, Jeshi la Polisi na Wataalamu wa elimu katika Shule ya Sekondari Kasingirima na Kasimbu.
Akizungumza kwa nyakati tofauti katika uhamasishaji huo Afisa maendeleo ya jamii kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Bi. Aida Nzowa amesema Wanafunzi wa kike wana uwezo mkubwa wa kufanya vizuri katika ujifunzaji.
Amewataka kujiamini, kuthubutu, uwajibikaji na kuchukua hatua na kuuliza kama njia ya kujifunza.
Kwa upande wake Afisa Dawati la Jinsia na Watoto Jeshi la Polisi Sanjenti Faraja Mkuya amewataka Wanafunzi hao kujiepusha na vitendo vya ngono ili kufikia malengo waliyokusudia.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kasingirima Ndugu. Venance Pastory Ndegea amewasisitiza Wanafunzi hao kuyaishi na kuyafanyia kazi nasaha zilizotolewa na Wataalamu hao.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa