Na Mwandishi Wetu
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amewataka Walimu wa MEMKWA kutumia mbinu za kiubunifu katika ufundishaji wa Wanafunzi wao.
Ameyasema hayo Leo Februari 13, 2026 alipowahutubia katika mafunzo ya Siku tano (05) yanayoendelea kuhusu malezi,unasihi na ulinzi wa mtoto yakifanyikia Shule ya Msingi Muungano.
Mkuu huyo wa Wilaya amewataka kufundisha kwa ufanisi na weredi kutokana na mazingira yao awali ya kuacha masomo kutokana na sababu mbalimbali.
Aidha amewataka Walimu hao kujiendeleza katika taaluma zao ili kuendelea kuwanufaisha Wanafunzi na Wananchi katika maeneo yao.
Akizungumza katika Mafunzo hayo Afisa elimu Watu wazima Ndugu. Cornel Kisinga amempongeza Mkuu huyo wa Wilaya kwa nasaha alizozitoa kwa Walimu huku akiahidi kufanyia kazi katika kuinua viwango vya ufaulu kwa Wanafunzi hao.
Mafunzo hayo yanafadhiliwa na Shirika la Kimataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) yakilenga kuwarejesha Wanafunzi walioacha masomo kutokana na sababu mbalimbali na kuwajengea Walimu mtazamo chanya kuhusu Ulinzi wa mtoto, kuimarisha huduma za malezi na unasihi.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa