Na Mwandishi Wetu
Mkuu wa wilaya ya kigoma Dr. Rashid Chuachua amewataka Wakuu taasisi za Serikali kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuendelea kutekeleza miradi ya Maendeleo.
Ameyasema hayo Leo Februari 13, 2026 katika kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya (DCC) cha kujadili rasimu ya mpango na bajeti kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 katika ukumbi wa Kigoma Social Hall.
Akiwasilisha makisio ya bajeti ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa niaba ya Mkurugenzi, Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu Ndugu. Julius Ndele amesema kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 Halmashauri imepanga kukusanya kiasi cha zaidi ya billion arobaini na nne (Tsh 44,944,875,400/=).
Amesema kiasi hicho kinakisiwa kukusanywa Mapato ya ndani yakiwa zaidi ya billion tano ( Tsh 5,985,756,400/=), Matumizi ya kawaida yakiwa zaidi ya billioni moja (1,618,040,000/=), mishahara ikiwa ni zaidi ya bilioni ishirini na Saba ( 27,667,312,000/=) na fedha ya miradi ya Maendeleo kutoka Serikali Kuu ikiwa ni zaidi ya billioni tisa ( Tsh 9,673,767,000/=) kwa ongeko la zaidi ya Millioni Mia mbili ( Tsh 223,960,400/=) Sawa na Asilimia moja (1%) ukilinganisha na makisio ya bajeti kwa Mwaka 2025/2026.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa