Na Mwandishi Wetu
Ujenzi wa Soko la kisasa katika Mwalo wa Kibirizi uliopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji umeanza kutekelezwa ukiwa katika hatua ya kujaza udongo na kutoa maji.
Ujenzi huo unatekelezwa ikiwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Sita Dr. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa alipofanya ziara Mkoani Kigoma.
Ujenzi huo unatekelezwa kwa gharama ya fedha za Kitanzania Billion Saba (Tsh 7,000,000,000/=) na Kampuni ya KGG Investment Limited kwa kipindi cha Mwaka mmoja.
Ujenzi wa soko hilo unajengwa kwa kuta za kubwa za kuzuia maji ya ziwa (Gabions) ukilinganisha na Soko lililokuwepo awali lililoathiriwa na maji.
Soko hilo linatarajiwa kuwa na maduka, Ofisi za Soko, Majengo ya Wajasiriamali wa Chakula, Vyoo na Kituo cha Polisi ukienda sambamba na ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami katika eneo hilo.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa