Na Mwandishi Wetu
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma Ndugu. Jamar Tamimu amepongeza Serikali kwa namna inavyotekelezaji mradi wa ujenzi wa Soko la Mwanga lililopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
Pongezi hizo amezitoa Leo Februari 02, 2026 alipokagua ujenzi huo akiambatana na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Kigoma kukagua Utekelezaji wa ilani ya Chama hicho.
Amewapongeza Wataalamu na wajenzi kwa namna wanavyosimamia ubora wa jengo huku akiwataka kukamilisha kwa wakati ili kuanza kuwanufaisha Wafanyabiashara.
Akiwasilisha taarifa Mhandisi wa Ujenzi kutoka Kampuni ya ujenzi ya Asabhi contractor Company Ltd in Jv with Pioneers Builders Limited Eng. Joseph Marando amesema utekelezaji wa Mradi umefikia asilimia sitini na moja (61.63%) huku akisema mwezi April Mwaka huu wanatarajia kukabidhi Mradi.
Aidha Wajumbe wa Kamati ya Siasa CCM Mkoa wametembelea na kukagua ujenzi unaoendelea wa chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi Muhimbili tawi la kigoma (MUHAS).
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tzt5
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa