Na Mwandishi Wetu
Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigoma imepongeza na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji.
Pongezi hizo amezitoa Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigoma Ndugu. Sadick Kibwana Kaduro katika ziara ya Kamati ya siasa ya Chama hicho iliyofanyika Leo Januari 29,2026.
Amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeridhishwa na namna miradi ya maendeleo inavyotekelezwa na kusimamia na Wataalamu ili kuwanufaisha Wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dr. Rashid Chuachua amewashukuru Viongozi hao huku akisema Wataalamu wataendelea kusimamia miradi ya Maendeleo kikamilifu ili iweze kuwanufaisha Wananchi.
Miradi iliyokaguliwa na kutembelewa ni Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Ujenzi wa Kituo cha afya cha Rusimbi, Ujenzi wa mfereji wa maji ya mvua Katubuka, ukaguzi wa Ujenzi wa Uwanja wa ndege, Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Kipampa, na kukagua Ujenzi wa Soko la Kisasa Mwanga.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa