• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

ANWANI ZA MAKAZI KURAHISISHA HUDUMA ZA MAENDELEO KWA JAMII, Postcode

Posted on: February 22nd, 2022

Na Mwandishi Wetu

Kukamilika kwa zoezi la anwani za makazi kutarahisisha Serikali  kufikisha huduma za maendeleo na manunuzi ya Kidigitali kwa Wananchi

Ameyasema hayo Mratibu wa zoezi la ukusanyaji wa anwani za Makazi Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Haji Omary Mwilima leo Februari 22, 2022 alipokuwa katika kipindi cha #Goodmorning Kigoma kinachorushwa  kila siku asubuhi na Radio joy 90.5

Mratibu huyo amesema kukamilika kwa zoezi hili kutafanya Serikali kuwa na takwimu sahihi  ya maeneo yanayohitaji  huduma za kijamii kama vile afya, elimu, na miundombinu mbalimbali ambazo  Wananchi   wa eneo husika wanahitaji ikiwa ni pamoja na kurahisisha upelekaji wa huduma hizo

Ameendelea kusema  kukamilika kwa zoezi hilo kila Mtanzania atakuwa na anwani halisi ya Makazi yatakayosaidia kila mtu kupatikana kirahisi, utambulisho wa watu, usajili wa biashara na mali na kuboreshwa kwa taarifa ya vizazi na vifo katika jamii

Kukamilika kwa zoezi hilo pia kutusaidia kufanyika kwa biashara mtandaoni ambapo Wafanyabiashara na wanunuzi watakuwa na uwezo wa kununua na kumfikishia mteja bidhaa, upatikanaji wa huduma za dharura kama vile polisi, huduma za zima moto kwa   uharaka kutokana na uwepo wa anwani na taarifa kamili za kila mtu    

Amesema zoezi hilo litafanyika kwa kutoa namba ya anwani ( namba ya jengo, au kiwanja),  majina ya barabara au kitongoji   na postikodi

Aidha ameendelea kusema hadi sasa tayari Makundi mbalimbali yamepata mafunzo ya namna zoezi hilo litakavyofanyika wakiwemo Madiwani, Watendaji kata na Mitaa na uelimishaji huo unatarajia kufanyika kwa Wenyeviti wa Mitaa na vijana  watakaohusika katika zoezi hilo

Amehitimisha kwa kuwataka Wananchi, Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kushiriki kikamilifu na kutoa ushirikiano wa watakaokuwa wakikusanya taarifa hizo wakishirikiana na viongozi wa kata na mtaa





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa