• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

ELIMU YA KUJIKINGA NA CORONA YAANZA KUTOLEWA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KWA MAKUNDI,YAANZA KUTOLEWA KWA WALIMU NA WANAFUNZI, Corona Virus

Posted on: March 16th, 2020

Na mwandishi wetu

Manispaa ya Kigoma/Ujiji leo march 16, imeanza kutoa elimu ya namna ya kujikinga na ugonjwa wa Corona katika taasisi za shule kwa Walimu na Wanafunzi kutokana na ugonjwa huo kuenea kwa kasi katika nchi mbalimbali duniani

Wataalamu kutoka idara ya afya ya manispaa hiyo wametoa elimu ya namna ya kujikinga na ugonjwa wa Corona kwa shule 5 za msingi na sekondari ambapo pia walimu wakuu wa shule zote za msingi, walimu wa afya mashuleni na waratibu Elimu kata wamepata elimu hiyo

Wakiwa katika uelimishaji  huo Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dk Siwale amewataka walimu na wanafunzi kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo kwa kuepuka baadhi ya matendo yaliyozoeleka katika jamii kama kusalimiana kwa kupeana mikono na kukumbatiana

Aidha Mganga Mkuu huyo amesema ugonjwa huo  kwa sasa hauna chanjo wala tiba ya moja kwa moja , na matibabu yanayofanyika ni kwa kuzingatia dalili zinazojitokeza na ufuatiliaji kwa ukaribu na ugonjwa huo huambukizwa kwa njia ya hewa au kugusa majimaji au kamasi kutoka kwa mtu mwenye virusi vya korona

Naye Dk Shabani Magorwa amesema dalili za ugonjwa huo wa corona ni kukohoa, homa kali, kuumwa kichwa, mwili kuchoka, vidonda kooni, maumivu ya misuli, na kupumua kwa shida hali inayoweza kupelekea umaiti kwa mtu mwenye dalili hizo

Amewataka walimu kuwa makini  na wanafunzi wao kwa kuwataka kunawa mara kwa mara baada ya kushika na kugusa kitu chochote na kuwataka walimu kutoa taarifa mara baada ya kuona mtu mwenye dalili hizo ili kuweza kupewa huduma mara moja na timu iliyoandaliwa manispaa ya Kigoma/Ujiji

Aidha Mganga mkuu huyo amewataka walimu kuendelea kutoa elimu zaidi kwa wanafunzi na walimu wengine ambao hawakupata elimu hiyo na hatimaye elimu hiyo kuifikia jamii kwa kila mmoja kuwa barozi wa utoaji elimu hiyo

Naye Kaimu Afisa elimu wa Manispaa hiyo Bi. Gunaguje ameshukuru elimu hiyo iliyotolewa na wataalamu kutoka idara ya afya na kusema maelekezo yaliyotolewa watayasimamia na kuhakikisha kila shule inakuwa na vyombo vya usafi vya unawaji katika shule zote na kusema kupitia elimu hiyo iliyotolewa kwa walimu na wanafunzi jamii kubwa ya wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji itatolewa na kwa watu wengine

Nao baadhi ya walimu waliohudhulia  katika elimu hiyo akiwemo Madamu Suzana  na mwalimu Julius Zackaria wameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa kuratibu elimu hiyo kwa lengo la tahadhari la ugonjwa huo wa Corona

Nao wanafunzi wa shule ya sekondari Bishop Kahurananga Godfrey Danga na Suzana Elikana wameshukuru wataalamu hao kwa kuwapelekea elimu hiyo huku wakisema maelekezo waliyopata namna ya kujikinga na ugonjwa huo watayafanyia kazi na kuwa mabalozi kwa wanafunzi wengine na jamii yote kwa ujumla

Mganga mkuu wa Manispaa hiyo amehitimisha kwa kuwashukuru walimu, wanafunzi na waratibu elimu kata kwa kuonesha ushirikiano wao na kusema elimu hiyo waliyoianza kuitoa ni endelevu ili kupambana na ugonjwa huo wa Corona kwa kata zote, mitaa na itafanyika katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi kama vile sokoni, mashuleni na maeneo ya starehe

Tayari Manispaa ya Kigoma/Ujiji imeshaanda eneo na wataalamu wa kuwahudumia wagonjwa hao kwa kuwapatia mafunzo endapo mgonjwa wa Ugonjwa huo atagundulika kuwepo, Na tayari vifo  3,217 vimelipotiwa nchini China huku vifo 1,809 nchini Italia Tangu ugonjwa huo kugundulika

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa