• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KAMATI YA SIASA YA CCM WILAYA YA KIGOMA YAFANYA ZIARA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA HICHO MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, YAWATAKA WATAALAMU KUTOZALISHA KERO KWA WANANCHI, CCM visit

Posted on: March 12th, 2020

Na Mwandishi wetu

Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Kigoma jana march 12, ilifanya ziara Manispaa ya Kigoma/Ujiji kukagua utekelezaji wa Ilani ya chama huku wakiwaasa Wataalamu wa Halmashauri hiyo kutozarisha kero na  kuwasumbua wananchi katika utoaji wa huduma

Aliyasema hayo Katibu Mkuu wilaya ya Kigoma wa Chama hicho Ndugu. Jumanne Kitundu alipokuwa katika kukagua miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kwa kipindi hiki cha serikali ya Awamu ya Tano

Alisema katika utendaji kazi wa watumishi wa serikali zipo taarifa za baadhi ya watumishi kutotoa huduma kwa wananchi kwa uzuri hivyo watumishi hao kutumia lugha zisizositahiri katika maeneo yao ya kazi na kuleta huduma mbovu serikalini na wengine kuzalisha matatizo au kero kwa wananchi

Aliendelea kusema  “Ninyi watumishi mnapaswa kuwa waamifu katika kazi zenu za kila siku mnazozifanya, na taarifa tunazo kwa wasiowaamifu na mnaotoa lugha zisizo sahihi na wengine kutumia mda mwingi bila sababu kutoa huduma jambo ambalo halikubaliki, Niwatake ninyi kama Watumishi tumieni maadili yenu ya kazi kufanya kazi kwa uaminifu ili tufike pale tunapotarajia kufika kama Watanzania”

Wakiwa katika eneo la Mlima Masanga ambapo ni chanzo cha mapato cha madini ya Manispaa hiyo Afisa Mapato Ndugu . Amoni  Ndakize alitoa taarifa na kueleza kuwa chanzo hicho kwa mwaka 2019 kimeingiza zaidi ya Fedha za Kitanzania Shilingi  Millioni Moja(1,000,000/=) licha ya changamoto ya namna watoza ushuru wanavyokusanya kutokana na ukubwa wa mlima huo

Wakiwa katika kitalu cha michikichi eneo la Katosho Mkuu wa idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Ndugu. Haruna Mtandanyi akitoa taarifa alisema kwa sasa Manispaa  imejikita katika uzalishaji wa miche ya michikichi kutokana na sera ya kuinua zao hilo na kusema  lengo la kuzalisha miche  milioni moja laki saba na elfu hamsini(1,750,000) ambapo michikichi hiyo itagawiwa kwa wananchi pasipo gharama yeyote

Aliendelea kusema hadi sasa miche elfu kumi na moja (11,000) tayari ipo katika viliba na mbegu zaidi ya elfu thelathini(30,000) zimesha zalishwa katika vitalu ili kuweza kuhamishia katika vitalu ambapo hadi kufikia mwezi Desemba, 2020 miche hiyo itakuwa tayari kusambazwa kwa wananchi na wakulima ambapo itakuwa na uwezo wa kuzalisha Tani 4 za mafuta ya mawese kwa hekari kwa mwaka tofauti na michikichi ya sasa  yenye uwezo wa kuzalisha Tani 1.5 kwa hekari kwa mwaka



Aidha wajumbe hao wa kamati ya siasa  wakitoa maoni yao katika ziara waliyoifanya, Katibu Mwenezi wa wilaya (CCM) Ndugu. Haruna Kambilo ameipongeza serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendelea kuleta miradi mbalimbali katika Manispaa hiyo na kuwapongeza wasimamizi  ambao ni wataalamu

Aliendelea kutoa ushauri kuwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika ukusanyaji mapato ihakikishe pia inarudisha maendeleo kwa kuboresha miundombinu katika vyanzo inavyokuwa inakusanya huku akitaka katika uchimbaji wa madini mlima wa Masanga kuweka miundombinu imara ya barabara ya kuwezesha usafirishaji na kuwapa mikopo wachimbaji hao ya vifaa vya uchimbaji

Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu.Frednand Filimbi katika ziara hiyo aliipongeza kamati ya siasa ya chama hicho kwa ziara waliyoifanya huku akiahidi kutekeleza ushauri walioutoa na kuendelea kutekeleza na kusimamia ilani ya Chama hicho

Katika ziara hiyo  miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ukarabati wa shule ya sekondari Lubengera unaoendelea, Machinjio ya Kibirizi na Ujiji, Soko la samaki la Kibirizi, Dampo la Kisasa Msimba,barabara 8 zilizojengwa chini ya mradi wa TSCP zenye urefu wa Km 11.97, eneo la soko la samaki soko la Kigoma mjini, ujenzi wa Zahanati unaoendelea eneo la Buronge, Makumbusho ya Dr.Living stone Ujiji, stesheni ya Kimoja, na barabara ya Katonga inayoendelea kujengwa kwa kiwango cha lami.

ingia katika maktaba ya picha kuona picha zaidi ya ziara hiyo

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa