• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

"KAMPENI YA TWENDE PAMOJA UKATILI KIGOMA SASA BASI" YAZINDULIWA MKOANI KIGOMA, against violency

Posted on: December 21st, 2021

Na Mwandishi Wetu

Katibu tawala wa Mkoa wa Kigoma Leo Desemba 21, 2021  amewataka wakazi wa Mkoa huo kujenga tabia ya kuripoti vitendo vya ukatili vinavyoweza kutokea ndani ya jamii

Ameyasema hayo katika uzinduzi wa Mwongozo wa  kampeni  ya kupinga ukatili iliyofanyikia Ukumbi wa Redcross   Manispaa ya Kigoma/Ujiji ikienda kwa jina la Twende Pamoja ukatili Kigoma sasa basi

Akihutubia katika ukumbi huo amewataka wakazi wa Mkoa huo kuwa na tabia itakayosaidia kutokomeza vitendo vya ukatili katika jamii kwa   kutoa taarifa katika  taasisi za Serikali  kama vile Dawati la Jeshi la Polisi,  Ofisi za Ustawi wa Jamii, Ofisi za Kata na Mitaa ili kutokomeza vitendo hivyo    

Katibu tawala huyo  ameyataka Mashirika ya Serikali na yasiyo ya Serikali kuendelea kuelimisha  jamii kupitia makundi ya watu wengi  na vyombo vya habari ili kuwa na jamii yenye Mazingira yaliyo salama katika shughuli za Kiuchumi za kila siku

Aidha amewataka Wazazi na Walimu kusimamia maadili ya watoto na kuwaepusha na maudhui ya mitandao ya kijamii yasiyokuwa na maadili ambayo yanaweza kusababisha ukatili na vitendo viovu ndani ya jamii

Amewataka viongozi wa dini kuendelea kuelimisha waumini kuwa na hofu ya Mungu na kuepukana  na vitendo ambavyo ni kinyume na maadili ya jamii  huku waganga wa jadi wakitakiwa kufanya kazi kwa uaminifu na kutokutoa maelekezo yanayoleta athari ya vifo na maumivu ndani ya jamii

Aidha amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Kigoma kuimarisha kamati za Kupinga Ukatili wa Kijinsia kwa Wanawake na Watoto (MTAKUWWA)  na kuwa na vikao vya Mara kwa Mara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kutokomeza vitendo hivyo vya ukatili

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia- Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Mwajuma Magwiza  amesema katika Mwongozo uliozinduliwa mambo   yanayosisitizwa ni pamoja na  Kuimarisha Uchumi wa Kaya,  jamii   kuepuka Mila na desturi potofu na kuweka Mazingira salama Mashuleni na Majumbani kwa watoto na wanafunzi

Ameendelea kusema Mpango wa MTAKUWWA una  lengo la  kupunguza  vitendo vya ukatili hadi  kufikia asilimia Hamsini (50%) huku akisema anaamini mwongozo wa kampeni ya Twende pamoja kupinga Ukatili Kigoma kama ukitumiwa kikamilifu utasaidia   kutokomea kwa vitendo hivyo Nchini

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Kigoma Ndugu. Elisha Nyamara amesema tangu Mwaka 2018 ambapo Mpango wa Kupambana na Vitendo vya ukatili wa Kijinsia na watoto ulipozinduliwa jumla ya Askari Mia moja kumi na tano (115) wamepatiwa mafunzo ya kupambana na vitendo vya ukatili, wahanga wa vitendo vya Ukatili elfu moja Mia moja kumi na nne (1114) wakipatiwa msaada na usaidizi na kisheria huku wataalamu wa afya Mia moja na thelathini (130) wakipatiwa mafunzo namna ya kuwahudumia waathrika na vikao vya kamati ya MTAKUWWA vikifanyika kila mwaka

Nao baadhi  ya washiriki wa Semina hiyo  Mwalimu Gervas Rwaho  na Mjasiriamali Bi. Beatrice Mtesigwa wamesema jamii ina amejibu wa kufuatilia vitendo vya ukatili na kukemea ili kuwa na jamii yenye iliyo sitarabika  

Mkutano huo Umehudhuria na  wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa dini, Wanazuoni,  waganga wa Jadi, Wazee na Viongozi Maarufu, Makundi ya Wanawake na vijana, Jeshi la Polisi , vikundi vya sanaa, walimu wa Msingi na Sekondari , waandishi wa Habari na watumishi wa idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii  



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa