• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KISHINDO CHA MWAKA MMOJA WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, MABILION YATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: March 20th, 2022

Ni mwaka mmoja sasa tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuapishwa kwake March 19, 2021 kuwa Rais wa Nchi baada ya kifo cha aliyekuwa Rais Mhe. John Pombe Magufuli alipofariki March 17, 2021

Mara baada ya Kuapishwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alianza kutekeleza na  kusimamia  miradi mbalimbali Nchini Kupitia Wizara na Taasisi mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kulinda Katiba ya Nchi

Kwa kipindi cha Mwaka Mmoja cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameendelea na utekelezaji  wa shughuli za Serikali na usimamiaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Wizara mbalimbali na kufanya  Mikoa na Halmashauri kunufaika na miradi  ya maendeleo kutokana na mapato ya ndani, fedha za wahisani na fedha kutoka Serikali Kuu

Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni miongoni mwa wanufaika wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka mmoja wa  Awamu Sita ikiwa ni pamoja na Ustawi wa Jamii katika sekta mbalimbali

SEKTA YA ELIMU

Katika sekta ya Elimu zaidi ya Tsh Billion 2 zimepokelewa Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika kipindi hiki cha mwaka mmoja wa Awamu ya Sita kwa idara ya Elimu Msingi na Sekondari

Idara ya Elimu Msingi Manispaa ya Kigoma/Ujiji  imepokea zaidi ya Tsh Million 260 ili kutekeleza miradi ambapo kiasi cha Tsh 180,000,000/= zimetumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa  tisa(09) katika Shule za Msingi Benjamini Mkapa (2) , Butunga (2), Mwasenga (2), Mlole (2) na shule ya Msingi Kipampa (1)

Aidha utekelezaji huo umeendelea kwa ujenzi wa matundu ya vyoo sitini (60) kwa kiasi cha Tsh 66,000,000/= kwa Shule za Msingi Mlole (6), Mwasenga (6), Butunga (12), Kiheba (12), Majengo (12) na Shule ya Msingi Mwasenga (12)

Mradi mwingine uliotekelezwa kwa Idara ya Elimu Msingi ni wa kujikinga na kupambana na athari za Uviko-19 kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi ambapo Zaidi ya Tsh Miillion 20 zilitumika kujenga miundombinu ya ujenzi wa kunawa mikono kwa Walimu na Wanafunzi Shule ya Msingi Mwasenga na Butunga zilizopo katika Manispaa hiyo

Idara ya elimu Sekondari Manispaa ya Kigoma/Ujiji Kwa kipindi cha Mwaka mmoja cha  Mhe. Rais imepata fedha za miradi ya maendeleo Zaidi ya Billion 2 jumla ya  madarasa hamsini na tisa (59) yamejengwa ambapo Madarasa arobaini na nane (48) yamejengwa kwa Shule mbalimbali  na kukamilika kwa kiasi cha Tsh 960,000,000/= katika mradi wa kupambana na athari za Uviko-19 ambapo ulifanikiwa kutoa ajira 414 na kuwanufaisha Wanafunzi 2400 ambapo hadi sasa madarasa yanatumika,   na ujenzi wa madarasa nane (08) katika Shule za Sekondari Buronge (02), Bushabani (02), Masanga (02) na Shule ya Sekondari Gungu (02)

UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI

Aidha kwa kipindi hiki cha mwaka mmoja Cha Utawala wa  Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan fedha ya awali  kwa ajili ya Ujenzi wa Shule mpya katika kata ya Businde imetolewa kiasi cha Million 470/= na Shule hiyo inatarajia kukamilika kwa kiasi cha Millioni 600/= ambapo awali Kata hiyo haikuwa kuwa na Shule ya Sekondari, miradi mingine ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa Maabara kwa Shule za Sekondari kumi na moja (11) kwa gharama ya Tsh Million 330/= na ujenzi wa matundu ya vyoo kumi na moja (11) kwa shule ya Sekondari  Masanga


SEKTA YA AFYA

Katika Sekta ya Afya, kwa kipindi cha Mwaka mmoja cha Utawala wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan Manispaa ya Kigoma/Ujiji imepokea zaidi ya Tsh Million 610/= ambapo kiasi cha Tsh 250,000,000/= tayari imepokelewa  kwa lengo la ujenzi wa Zahanati ya Buhanda ikiwa ni fedha ya awali na kituo hicho kinatarajia kukamilika kwa Tsh Million 600/= ikiwa ni fedha kutokana na tozo ya Miamala ya Simu

Fedha zingine zilizopokelewa kutoka Serikali Kuu  ni Tsh 250,000,000/= za ujenzi wa jengo la Wagonjwa wa Nje (Opd) katika kituo cha afya cha Gungu,  ujenzi wa uzio katika zahanati ya Msufini kwa gharama ya Tsh million 35/=, ujenzi wa uzio wa zahanati ya Kigoma kwa gharama ya  Tsh Million 35/=, ujenzi wa uzio wa Zahanati ya Buhanda kwa gharama ya Tsh Million 45/=, na  ujenzi wa uzio wa zahanati ya Businde kwa gharama ya Tsh Million 45/=  ambapo kukamilika kwa ujenzi huo kutasaidia ulinzi katika maeneo ya vituo hivyo, upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi na haraka

MIUNDOMBINU YA BARABARA

katika uboreshaji wa miundombinu ya barabara Serikali ya Awamu ya Sita ikiongozwa na  Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha Mwaka mmoja  Manispaa ya Kigoma/Ujiji chini ya usimamizi wa  TARURA  imepokea  zaidi ya Billion 2 na kuongeza Mtandao wa barabara kutoka Km 324 zilizokuwepo awali na kufikia Km 336.51 hadi hivi sasa

Aidha Serikali Kuu imetoa kiasi cha Tsh Billion moja (1, 000,000,000/=) ambapo zimetumika katika ujenzi wa barababara ya Mabatini na Muungano B kwa kiwango cha lami ambapo jumla ya Km 0.8 zimejengwa, ujenzi wa barabara ya Muungano Km 2.01 ( starehe-Kilimahewa), na barabara ya Mlimani 0.5 km na Mitalo kwa kiwango cha changarawe

Fedha zingine ni Billion 1. 05 zimeendelea kutekeleza ujenzi wa barabara kwa matengenezo ya kawaida Km 93.3, Matengenezo ya Maeneo korofi Km 1. 56 na Matengenezo ya Mda Maalumu Km 0.63, ambapo Ujenzi wa huo wa barabara,  mifereji, kalvati na Madaraja unaendelea katika Kata mbalimbali za Manispaa hiyo

HUDUMA YA MAJI

 Mamlaka ya Maji Manispaa ya Kigoma/Ujiji (KUWASA) kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita imefanikiwa  kuongeza Mtandao wa mabomba ya Maji wenye jumla ya Km 62. 2 kwa gharama 599, 962, 060/= ambapo hadi sasa kiasi cha Tsh Million 200/= imepokelewa  kwa ajili ya ununuzi wa bomba na vifaa vya km 18 katika maeneo ya Busomelo, Kagera, Kigamboni, Bushabani, Kibirizi, Bangwe na Buronge na inatarajiwa kufanyika Kilimahewa, na Gungu

ANWANI ZA MAKAZI

Manispaa ya Kigoma/Ujiji tayari imepokea zaidi ya fedha Kiasi cha Million 97/= kutoka Serikali Kuu kwa lengo la utekelezaji wa mradi wa Anwani za Makazi ambapo hadi hivi sasa Utekelezaji huo unaendelea na mradi huo utasaidia Kila Mkazi wa Manispaa hiyo kutambuliwa na kurahisisha upatikanaji wake , uwekaji wa Namba za Nyumba, Majina ya Mtaa na Postikodi ambapo kukamilika kwake kutusaidia kukuza na kuboreshwa kwa huduma za Ulinzi na Usalama ndani ya Jamii, kufanyika na kukuza  kwa biashara Mtandaoni kidigitali na Kusaidia Serikali kufikisha huduma kwa wananchi kirahisi kulingana na Mahitaji ya eneo husika

MRADI MPYA

Mradi mwingine unaotarajia kutekelezwa ni wa kuendeleza na Kukuza Miji na Majiji Kimkakati (TACTICs) ambapo ujenzi wa barabara mbalimbali kwa kiwango cha lami unatarajiwa kufanyika Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambapo zaidi ya Km 15 zinatarajiwa kujengwa,  Ujenzi wa Kisasa soko  la Mwanga, Ujenzi wa Kisasa wa Soko la mazao ya Uvuvi Katonga, Ujenzi wa miundombinu ya Mifereli ya Maji ili kudhibiti athari zitokanazo na mmomonyoko ambapo Mtalo Burega, Bushabani, Mji Mwema,  Katonyanga na Mlole mifeji hiyo inatarajiwa kujengwa ili kudhibiti athari kwa Wananchi

Hivi Karibuni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akihojiwa na baadhi ya vyombo vya habari vikiangazia Utekelezaji wake kwa kipindi cha Mwaka mmoja wa Utawala wake alisema ataendelea na Utekelezaji wa Miradi Mbalimbali ya Kimaendeleo ili kukuza Uchumi wa Nchi, Kuzalisha ajira na kuongeza Ustawi wa Maisha ya Watanzania katika kipindi chote cha Utawala wake

Picha na ya miradi mbalimbali iliyotekelezwa inapatikana katika maktaba ya picha kupitia tovuti ya www.kigomaujijimc.go.tz na mitandao yetu ya kijamii 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa