• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KONGAMANO LA UWEKEZAJI MKOANI KIGOMA LAZINDULIWA, FURSA MBALIMBALI ZAJADILIWA. Bussines Conference

Posted on: May 9th, 2019

Na Mwandishi wetu.

Naibu waziri wa Tamisemi Mhe. Josepahati  Kandege leo  may 9, amezindua kongamano la uwekezaji mkoani Kigoma linalozungumzia fursa mbalimbali zilizopo mkoani hapo.

Katika kongamano hilo liliofanyika katika ukumbi wa NSSF halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji wadau mbalimbali wamehudhulia wakiwemo wawakilishi kutoka nchi jirani nchi ya Burundi, Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Rwanda na Zambia ambapo wawakilishi kutoka mikoa jirani nayo wamehudhulia , mkoa wa Katavi na Kagera.

Akimkaribisha mgeni rasmi mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali  Emmanuel  Maganga alianza kwa kuwatakia pole Watanzania wote kwa msiba mkubwa uliolikumba Taifa kwa kifo cha Dr. Reginard Mengi.

Mkuu wa mkoa huyo amewakaribisha wadau mbalimbali kutoka mkoa wa katavi, kagera na wawakilishi kutoka nchi jirani huku akisema Kigoma ni eneo salama kiuwekezaji na nchi jirani ambazo zilikuwa na migogoro ya kisiasa, migogoro hiyo imepungua.

Akizindua kongamano hilo Naibu waziri wa Tamisemi kwa niaba ya Makamu wa raisI  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  amesema kongamano hilo ni la kwanza na la kitaifa ambalo kwa jina la Tanganyika Bussines  Summit and Festival na kushukuru ofsi ya mkuu wa mkoa  na Chamber ya Kibiashara (TCCIA), Local Investimate Climate( LIC)  na wadau wengine kwa kufanikisha maandalizi ya mkutano huo.

Amewataka wadau mbalimbali waliohudhulia kongamano hilo kuona fursa zilizopo mkoani hapo na mkutano mkubwa huo kuwanufaisha na kuhakikisha kushiriki kikamilifu ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu wa kibiashara baina ya wafanyabiashara  wa Tanzania na wafanyabiashara wan chi zinazozunguka ziwa Tanganyika.

Akizungumza katika kongamano hilo fursa zilizopo mkoani Kigoma Mshauri Mwelekezi wa uwekezaji  Ndugu. Osward Mashindano amesema “K igoma ina fursa nyingi na utajiri wa kutosha lakini bado wananchi sio matajiri na fursa hizo baadhi ya watu hawazifahamu”

Ameendelea kusema Kigoma ina wakazi zaidi ya milioni 2 jambo linalofanya kuwepo na soko la uhakika kibiashara na uwepo wa nguvu kazi katika masuala ya uwekezaji , ambapo amewakaribisha wadau mbalimbali wa ndani na nje kuja kuwekeza mkoani hapo.

Ameendelea kusema mkoa wa Kigoma una madini tofauti tofauti aina kumi jambo linalovutia wawekezaji katika soko hilo na hadi hivi sasa kuna masoko makubwa manne(4) yaliyoanzishwa  masoko 2 yakiwa wilaya ya Kankonko, soko 1 likiwa wilaya ya Buhigwe na soko lingine likiwa wilaya ya Kigoma.

Ameendelea kusema tayari mkoa umetenga eneo la uwekezaji kwa jina la  Kigoma development economic  zone ambapo wawekezaji walishapewa maeneo na  baadhi  wameanza kujenga miundombinu mbalimbali ya viwanda vya uchakataji wa mafuta ya mawese na korie ,na  mitambo ya umeme

Amehitimisha kwa kuwataka wadau mbalimbali kuja kuwekeza mkoani hapo katika kilimo cha miwa katika bonde la mto Ruiche, kilimo cha ufugaji nyuki kutokana na misitu iliyopo mkoani hapo wilaya ya Kibondo na kasulu na kuja kuja kufanya utalii katika  hifadhi ya Mbunga ya Mahare na hifadhi ya Gombe, kuwekeza katika ufugaji na uvuvi wa samaki kutokana na uwepo wa ziwa Tanganyika na kuwekeza katika usafirishaji  wa majini, nchi kavu na anga.

Aidha katika uzinduzi wa kongamano hilo umeenda sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachozungumzia fursa zilizopo mkoani Kigoma, kongamano linatarajiwa kufanyika kwa mda wa siku tatu kuanzia mei 9 hadi mei 11 katika kongamano hilo lililoandaliwa na ofisi ya mkoa wa kigoma na washiriki wakiwa ni wadau kutoka nchi na mikoa inayozunguka ziwa Tanganyika.  .

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa