• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2021 WILAYA YA KIGOMA, MAANDALIZI YAANZA, Uhuru Torch

Posted on: August 5th, 2021

Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Ulinzi na Usalama  Wilaya ya Kigoma leo August 5, 2021 imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi na njia pendekezwa itakayotumika katika ukimbizaji wa  Mwenge wa Uhuru unaotarajia kukimbizwa katika Wilaya hiyo Septemba 27, mwaka huu


Ziara hiyo imefanyika ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Ester Alexander Mahawe ambapo jumla ya miradi tisa (09) imetetembelewa huku miradi minne (04) ikipendekezwa kuwekewa mawe ya Uzinduzi, miradi miwili (02) ikipendekezwa kuwekewa mawe ya Msingi na Miradi mitatu (03) ikipendekezwa kukaguliwa na kutembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru

Miradi hiyo iliyopendekezwa Kwa Hàlmashauri ya Wilaya  ni pamoja na  kutembelea kiwanda kidogo cha wanawake  kilichopo eneo la Kijiji cha Simbo kikijihusisha na uzalishaji Mawese, Mise, na Mafuta ya Mise na gharama ya Mradi ukiwa ni fedha za Kitanzania Million kumi na Moja na laki sita(11,600,000/=) chanzo cha fedha ikiwa ni ufadhili mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu


Aidha miradi mingine ni pamoja na Uzinduzi wa Daraja la Nyabigufa lenye gharama ya Million mia moja na saba (107,000,000/=) lilipo Mkongoro , Uzinduzi wa mradi wa Maji Kijiji cha Matyazo kilichopo kata ya Kalinzi ukiwa na gharama ya Million mia tatu kumi na saba (317,641,513/=)


Miradi mingine pendekezwa kwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni pamoja na Kutembelea Kitalu cha Michikichi kilichopo eneo la Katosho ambapo Jumla ya  Miche laki moja na elfu kumi na sita imeshazalishwa (116,000) ikiwa imegharimu kiasi cha Million ishirini laki tano (20,500,000/=) na zaidi ya Miche elfu thelathini (30,000) imeshagawiwa kwa wakulima bure na mingine ikipandwa Kando ya barabara za mji    

Miradi mingine ni Uzinduzi wa Jengo la Kujifungulia wazazi na Upasuaji  Zahanati ya Gungu likiwa limegharimu kiasi cha Fedha Million mia mbili sabini (270,000,000/=), Uwekeaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi wa Machinjio ya Kisasa gharama ya Mradi ukiwa ni Million mia moja themanini na mbili (182,000,000/=), Uzinduzi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja  Shule ya Msingi Mwasenga vikiwa vimegharimu Million Sitini (60,000,000/=), Uzinduzi wa Maabara mbili kwa Shule ya Sekondari Mlole ukiwa umegharimu kiasi cha fedha Million arobaini na tisa laki tatu (49,300,000/=) na Utembeleaji wa chumba cha Tehama katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa

Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu wa 2021 ni Mbio maalum, umaalum wake pia unatokana na Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru kukimbizwa katika Wilaya za kiutawala tu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya Halimashauri za Wilaya kama ilivyozoeleka, Na Wilaya ya Kigoma Mwenge wa Uhuru unatarajia kupokelewa kutoka Wilaya ya Uvinza Septemba 27 na Kutembelea, kukagua na kuzindua miradi pendekezwa huku Septemba 28 ukikabidhiwa katika Wilaya ya Buhigwe


Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2021, unahusu matumizi sahisi ya TEHAMA, chini ya Kauli mbiu isemayo: “TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu .Itumie kwa usahihi na Uwajibikaji”. Pamoja na Ujumbe huo, Mbio za Mwenge wa Uhuru zitaendelea kuwakumbusha na kuwahamasisha wananchi na Viongozi kote nchini, kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI, Ugonjwa wa Malaria, mapambano dhidi ya matumizi ya Dawa za Kulevya, Mapambano dhidi ya Rushwa na kuhamasisha Wananchi juu ya Lishe bora kwa afya imara.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa