• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MIKUTANO YA MASUALA YA KIJAMII,MAZINGIRA NA MALALAMIKO YAANZA KATIKA HALMASHAURI YA KIGOMA UJIJI KATIKA MIRADI INAYOFADHILIWA NA BENKI YA DUNIA CHINI YA USIMAMIZI WA TSCP, WAKAZI WA MTAA WA UJENZI WAASWA KUTUNZA MAZINGIRA

Posted on: August 28th, 2018

Mratibu wa jamii na mazingira katika mradi wa uendeleaji miji ya kimkakati Tanzania au Tanzania Strategic Cities Project (TSCP) katika manispaa ya Kigoma/Ujiji bi. Agnes Sanga jana Agosti 23,  amewataka wananchi wa mtaa wa ujenzi manispaa ya Kigoma Ujiji kutunza miundo  ya barabara inayotarajiwa kujengwa hivi karibuni.

Ameyasema hayo katika mkutano uliofanyika katika soko la Nazarethi katika kutambulisha mradi wa ujenzi wa barabara hiyo ya Nazarethi yenye km 1.7 , katika mkutano huo wataalamu mbalimbali kutoka ofsi ya Mkurugenzi wa manispaa walihudhulia akiwemo Afisa malalamiko, afisa maendeleo ya Jamii na mratibu wa masuala ya UKIMWI manispaa ya Kigoma Ujiji, afisa mtendaji wa mtaa na wanakamati ya malalamiko ya kata na mtaa.

Akiendelea kuongea katika mkutano huo mratibu wa jamii na mazingira bi. Agnes Sanga amesema mradi huo unafadhiliwa na benki ya dunia na fedha zinazoletwa ni sehemu ya mkopo kwa wananchi hivyo wananchi hawana budi kuipenda miradi hiyo na kuweka mikakati mizuri ya kuweza kuitunza.

Mratibu huyo aliendelea kusema katika miradi hiyo inayotarajiwa kujengwa ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha usalama unakuwepo katika kipindi chote cha ujenzi wa barabara hiyo kwa kuhakikisha alama za usalama zipo katika maeneo yanayojengwa ili kuepuka ajali zinazoweza kujitokeza kwa kutoa taarifa katika ofsi za kata pindi wanapoona wajenzi hawakuweka alama hizo.

Aliendelea kuwataka wakazi wa mitaa hiyo kuhakikisha wanatunza mazingira na kuwa wasafi katika kipindi chote cha ujenzi na hata ujenzi utakapokuwa umekamilika kwa kuhakikisha mitalo inakuwa safi na kutotupa taka ovyo.

Lakini pia mratibu huyo aligusia suala la ajira kwa vijana , ambapo aliwataka vijana kuchangamkia suala la ajira kwa kuomba kufanya kazi zile zinzohusisha taaluma hata zile zinazotumia nguvu na kuacha kukaa vijiweni , alionya suala la ajira kwa watoto wadogo na kuwataka wakazi wa mtaa huo kuwa makini na suala la kuajiri watoto wadogo jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi na kusema endapo suala hilo litajitokeza wananchi wahakikishe wanachukua hatua kwa kutoa taarifa katika uongozi wa eneo husika.

Naye afisa malalamiko wa halmashauri Ndugu. Meleji Mollel  akiwa katika mkutano huo aliweza kutambulisha kamati ya malalamiko ya mtaa na kata kwa wakazi na kusema tayari kamati hiyo ipo kazini na yapo malalamiko ambayo tayari wameanza kufanyia kazi yakiwemo ya kukatwa kwa bomba la maji katika kazi za awali za wakandarsi ambazo wamekwishaanza nazo.

Afisa malalamiko huyo alisema katika kipindi cha ujenzi yataweza kutokea matatizo tofauti tofauti ambayo yatahitaji utatuzi , alisema ni bora matatizo hayo yafuate hatua kwa hatua kuanzia ngazi ya mtaa, kata hadi kufikia manispaa kwa lengo la kutatuliwa

Lakini pia afisa huyo aliendelea kusema malalamiko wanayoshugulikia ni ya pande zote si upande wa wananchi bali pia hata kwa wakandarasi wanaojenga barabara hizo kwani yapo matatizo mengi yanayosabaibishwa na wanachi katika ujenzi ikiwemo wizi wa simenti, matusi hata ugomvi kwa wakandarsi kwa watu wasiowavumilivu.

Naye mratibu wa Ukimwi katika mradi huo wa TSCP aliwataka wakazi wa mitaa hiyo kuwa na uhusiano mzuri na wageni watakokuja kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo lakini pia kuwa makini na mahusiano yatakayojengwa ambayo hayataweza kuleta athari za magonjwa ya zinaa na UKIMWI.

Aliendelea kusema kama mjenzi au mkandarsi anaweza kupendana na mwenyeji wa eneo hilo ni muhimu kufuata hatua za kupima kabla ya kushiriki tendo la ndoa na kuwataka pia kuweza kutumia kondomu kwa ajili ya kuzuia maambukizi hayo ya virusi vya Ukimwi.

Naye afisa maendeleo Ndugu. Radan Lameck  akiwa katika mkutano huo alisema ni fursa nzuri ya kimaendelea iliyojitokeza katika ujenzi wa barabara hiyo kwani itaweza kuleta mapinduzi chanya ya kimaendeleo ikiwa ni kuongeza thamani ya ardhi pamoja na makazi .

Aliendelea kusema wakazi wa manispaa wachangamkie fursa hiyo katika kufatilia ujenzi wa barabara yenye ubora  ili bara bara iwe imara kwani itaweza kusaidia madereva wa bodaboda na magari kuokoa fedha nyingi za matengenezo kwa kupita katika barabara iliyo imara.

Nao wananchi wa mtaa huo wa ujenzi wakiwa katika mkutano akiwepo Ndugu. Mussa Hamisi na  Yaredi Bada wameweza kupongeza kwa mkutano uliofanyika kwa kusema wamepata elimu ya kutosha juu ya mradi huo wa barabara unaojengwa na kuomba ajira zitakazotolewa zisije kutolewa kwa upendeleo wa aiona yeyote kwa wakazi wa eneo hilo.

Naye mratibu wa jamii na mazingira bi. Agnes Sanga  amehitimisha kwa  kuwashukuru wakazi wa mtaa huo kwa kuweza kujitokeza katika mkutano huo na kusema tayari wakandarasi wapo katika miradi na wameanza ujenzi hivyo wananchi watoe ushirikiano katika mradi huo wa barabara unaojengwa kwani mradi huo na barabara zingine zikiwemo ambazo ni barabara ya kakolwa , barabara ya kitambe mwembetongwa, barabara ya Burega, barabara ya Kagera  pamoja na mfereji wa mlole na katonyanga yote itajengwa kwa mwaka mmoja na miezi mitatu.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa