• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU NCHINI TANZANIA AWATAKA WAKAZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KUPANDA MICHE YA KISASA YA MICHIKICHI, Palm tree

Posted on: June 18th, 2021

Na mwandishi wetu

Mkurugenzi  Mkuu wa Takukuru Kamishina wa Polisi  Salum Rashidi Hamduni leo June 18, 2021 amepanda miche ya zao la Michikichi katika Shule ya Sekondari Kasingirima iliyopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji alipokuwa akihitimisha ziara ya siku tatu Mkoani Kigoma aliyoifanya kwa lengo la kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma

Mara baada ya kupanda miche hiyo Kamishina huyo ameipongeza Serikali kwa kuamua kuinua zao la michikichi huku akisema jambo hilo litaleta tija Nchini kwa kuwainua wakulima wa zao hilo kutokana na uzalishaji wa mafuta mengi ya mawese na kuwataka wakulima kupanda miche hiyo katika mashamba yao

 Aidha kiongozi huyo amefanya mazungumzo na Klabu ya wanafunzi wapiga rushwa waliopo katika shule hiyo huku akiwataka wanafunzi hao kuwa mfano mzuri wa kupinga viashiria na utoaji rushwa kwa kutoa taarifa katika mamlaka husika kuanzia ngazi ya Wilaya hadi Mkoa

Akitoa taarifa ya uzalishaji wa miche ya kisasa ya Michikichi Kaimu Mkuu wa Idara ya kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Ndugu. Haruna Mtandanyi amesema Serikali imeamua kuwekeza katika zao la Michikichi ya kisasa  itakayokuwa na uwezo wa kuzalisha ili kuzalisha tani nne(4) hekta kwa mwaka kutoka tani moja (1) hekta kwa mwaka  kwa michikichi iliyokuwepo

Ameendelea kusema lengo la Halmashauri ni kuzalisha miche million moja (1,000,000) na kuigawa kwa wakulima bure na hadi sasa miche elfu thelathini (30,000) imegawiwa kwa wakulima, kupanda kando ya barabara na kupanda kwa baadhi ya taasisi za Serikali huku akiongezea kuwa ifikapo mwezi oktoba wakulima watagawiwa miche zaidi ya laki moja (100,000)  bure

Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu.Frednand Filimbi amempongeza Kamishina Mkuu wa Takukuru Nchini kwa kuamua kupanda zao la Mchikichi katika shule ya Sekondari Kasingirima, huku akisema kupanda kwake huko kutaleta hamasa kwa wakulima,  jamii na wakazi wa Manispaa hiyo kuendelea kuona umuhimu wa kulima zao hilo

Viongozi wengine walioshiriki upandaji wa miche ya kisasa ya michikichi ni Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kigoma Stephen Mafipa, na Naibu wa Takukuru Mkoa wa Kigoma Nestory Gatawa





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa