• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA MKOA WA KIGOMA AFANYA ZIARA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KUFUATILIA AGIZO LA UJENZI WA MADARASA

Posted on: January 31st, 2020

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga jana Jnuari 30, alifanya ziara katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kufatilia utekelezaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari

Ziara hiyo aliyoifanya ikiwa ni kufuatilia utekelezaji wa agizo la Ofisi ya Raisi TAMISEMI kuwa kwa halmashauri za zenye upungufu wa vyumba vya madarasa nchini kufikia februali 29, ujenzi wa vyumba vya madarsa uwe umekamilika na wanafunzi kuanza  masomo yao mara moja

Katika ziara hiyo aliyoifanya akianzia katika Sekondari ya Buzebazeba , Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndugu. Mwailwa Pangani alitoa taarifa kuwa halmashauri ilikuwa inakabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarsa thelathini na nane (38) , ambapo jumla ya vyumba  kumi na moja (11) vipo tayari na vinaendelea kufanyiwa ukarabati ili wanafunzi kuweza kuanza masomo yao mapema mwezi march

Mkurugenzi huyo alisema vyumba  vnine (4) vya madarasa vimejengwa katika shule ya sekondari Buzebazeba ambayo ni shule mpya na tayari amekwisha kupokea usajili wa shule hiyo, na madarasa mengine saba (7)  yapo katika shule ya msingi Kigoma ambayo wanafunzi wamehama kutoka katika madarasa hayo na kuhamia katika madarasa mapya ambayo yameshajengwa tayari na kukamilika

Ameendelea kusema katika shule hiyo ya msingi madarasa hayo yaliyokuwa yakitumiwa na wanafunzi wa shule ya msingi yameombewa usajili ili yaweze kutumika kama shule ya sekondari  na tayari wadhibiti ubora wa elimu wamekubaliana na kutoa vigezo vya shule hiyo kusajiliwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa ukuta au uzio  wa kutenganisha shule hizo mbili ya msingi na  sekonadri

Aidha ameendelea kusema madarasa hayo yaliyokuwa ya shule ya msingi yanatarajiwa kufanyiwa ukarabati na  tayari kuanzia kesho fundi anatarijia kuanza ukarabati wa miundombinu hiyo ikiwa ni pamoja na ukarabati wa madarasa na miundombinu ya vyoo vya shule hiyo, na kusema shule zingine zenye upungufu wa madarasa tayari ofisi ya Mkurugenzi imenunua tofali laki nne na elfu arobaini na saba na mia tano (447500) ambapo tofali hizo zimesambazwa na zinaendelea kusambazwa katika shule ili kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa ishirini na saba (27)

Mkurugenzi huyo alihitimisha kwa kuwashukuru wananchi wa Manispaa hiyo kwa kuhamasishana kuchangia ujenzi wa   vyumba vya madarasa  kwa kutumia nguvu ya wananchi kwa hali na mali ambapo mikutano ya wananchi kwa baadhi ya kata ziliazimia kila kaya kuchangia kiasi cha Tsh 10,000/=, huku wakishirikiana na wataalamu wa kata, wenyeviti wa serikali za mitaa na wadau mbalimbali wa elimu

Naye mkuu wa mkoa akiwa katika ziara hiyo aliridhishwa na ujenzi wa shule hizo mpya za sekondari zinazojengwa huku akitoa ushauri wa kupandwa kwa miti katika sekondari ya Buzebazeba, na kuahidi kuendelea kufuatilia ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa na  akiahidi kutoa mifuko ya simenti kumi (10) katika shule ya sekondari Gungu kutokana na kuridhishwa na mikakati na miundombinu ambayo imeshawekwa katika shule hiyo

Aidha mkuu huyo wa mkoa alitembelea standi ya  magari makubwa ya mizigo aina ya malori inayojengwa katika halmashauri hiyo ikiwa ni agizo la mkuu huyo wa mkoa kutokana na uharibifu unaofanywa na magari hayo yanapoingia mjini kushusha mzigo huharibu kingo za barabara za mjini na kusema ujenzi wa standi hiyo itakuwa ni fursa kwa wasafirishaji wa magari madogo ya mizigo, bodabaoda, wapishi wa migahawa na nyumba za kulala wageni katika eneo hilo

Katika ziara hiyo aliyoifanya mkuu wa mkoa huyo alitembelea shule ya sekondari Buzebazeba, shule ya msingi Mnarani , shule ya msingi Buzebazeba,  shule ya Sekondari Rubengera, shule ya sekondari Buronge, shule ya sekondari gungu na standi ya magari makubwa ya mizigo lililopo kata ya Gungu, ambapo pia ameongea na walimu, wanafunzi na wananchi kero zinazowakabiri katika jamii yao

Picha na matukio zaidi tembelea maktaba ya picha ya www.kigomaujijimc.go.tz

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa