• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA ASEMA "KUKATIKA KATIKA KWA MAJI ITAKUWA HISTORIA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI, AZITAKA TAASISI NA IDARA ZA SERIKALI KUSIMAMIA MIRADI KWA WEREDI"

Posted on: October 11th, 2021

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe amezitaka Taasisi na Idara za Serikali kusimamia fedha za miradi zinazoletwa wilayani hapo zitumike kwa usahihi pasipo kuwa na ubadhilifu

Ameyasema hayo leo October 11, 2021 wakati akifungua Mkutano wa wadau wa Maji Manispaa ya Kigoma/Ujiji chini ya mradi wa uwazi na uwajibikaji katika sekta ya maji unaofadhiliwa na  Asasi ya Nyakitoto Youth For Development Tanzania(NYDT) uliofanyika  katika ukumbi wa Hotel ya Just in Time

Amesema amemuelekeza Katibu Tawala wa Wilaya kuwaandikia Taasisi na Idara zote za Serikali kupeleka taarifa ya fedha zote za miradi zilizopokelewa kutoka Serikalini na Wadau wengine wa Maendeleo kwa lengo la kuzimamia na kuhakikisha miradi iliyokusudia inatekelezwa kwa manufaa ya wananchi

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amesema kwa sasa ujenzi wa mradi wa Maji unaendelea kujengwa  ukiwa na uwezo wa Kuzalisha lita za maji Million mia moja na arobaini na Mbili (lita 142,000,000) na Matumizi yakiwa Lita Million mia moja ishirini na tatu (lita 123,000,000) kwa wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambapo tatizo la kukatika kwa Maji litakuwa limekwisha na maji mengine kutumika katika Vitongoji na Vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

Mkuu huyo wa Wilaya amekemea vitendo vya baadhi ya  watumishi  wa idara ya maji wasiokuwa waaminifu kuomba Rushwa kwa wateja wanaoenda kupata huduma ya kufungiwa maji majumbani na wengine kuwabambikizia wananchi malipo (Bill) kubwa kwa lengo la kujinufaisha huku akisema vitendo hivyo hatavifumbia macho pindi anapopata taarifa zilizo sahihi

Ameendelea kusema mradi huo  tayari umeanza kufanya kazi na wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji na wakazi wa Mji mdogo Mwandinga wameendelea kunufaika huku akisema tayari mkandarasi anaendelea kujenga kwa kipindi cha mwaka mmoja kutokana na Mkandarasi wa awali  kushindwa kukamilisha ujenzi huo

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa agizo la kutaka kuzifahamu Asasi zote zisizo za Serikali (NGO’s) zinazofanya kazi katika wilaya hiyo kwa lengo la kutambua shughuli na miradi inayotekelezwa kwa ajili ya kuwasaidia na kuwainua Wananchi wa Wilaya hiyo  huku akiipongeza asasi ya NYDT kwa uwazi na uwajibikaji wao

Diwani wa kata ya Mwanga Kaskazini Mhe. Sharon Mashanya  amesema kikao hicho kinatarajia kuleta tija kwa Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji  ya upatikanaji wa maji kutokana na ufatiliaji utakaokuwa ukifanyika kuanzia kamati za maji zilizoundwa na  wananchi ngazi za mitaa

Meneja mradi wa uwazi na uwajibikaji katika sekta ya Maji kutoka asasi ya Nyakitoto Youth For Development Tanzania  Ndugu. Ramadhani Joel amesema Mkutano huo wa wadau wa Sekta ya Maji umewakutanisha  kwa lengo la kujadili Fursa, changamoto na Mafaniko ya upatikanaji wa Maji katika Kata tisa za Manispaa hiyo mbapo mradi huo unatekelezwa

Mkutano huo umehudhuliwa na Wataalamu kutoka KUWASA, Ewura CCC, TANESCO, TAKUKURU, Madiwani, na kamati za Wananchi za Maji ngazi ya kata ambazo zimeweza kuunda kamati ndogo za ufatiliaji wa upatikanaji wa maji

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa