• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA USO KWA USO NA WAHANGA WA BWAWA LA KATUBUKA, ponds

Posted on: September 8th, 2021

Na Mwandishi wetu

Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Kigoma ikiongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo  Bi. Ester Mahawe leo Septemba 8, 2021 imefanya ziara na kukutana na wananchi  ambao ni wahanga wa bwawa la Katubuka liliojaa maji na kuathiri Makazi yao

Mkuu huyo wa wilaya ya Kigoma amewashauri wahanga hao kuondoka katika eneo hilo kabla ya athari kubwa kuelekea kipindi cha mvua na kutafuta maeneo mengine  huku akisema anaenda kukutana na wataalamu kuona namna gani ya kuwasaidia wananchi wa eneo hilo ili kuepukana na maafa yanayoweza jitokeza

Kaimu Mkuu wa idara ya Mipango miji, Ardhi na Maliasili Ndugu. Steven Ambrose amesema katika kipindi cha miaka ya nyuma (1990s) idara ya ardhi Mkoa wa Kigoma ilipima viwanja katika eneo hilo na kugawiwa  kwa wananchi na baadae eneo hilo kuanza kujaa maji huku mwaka 1995s Wakazi wa eneo hilo wakipewa fidia na kutakiwa kuhama licha ya wengine  kukaidi agizo hilo na kuanza kuuza viwanja kwa watu wengine ambao ni waathirika kwa sasa

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwanga ambapo bwawa hilo linapatikana Ndugu. Mfaume Kimeya amesema  historia inaonesha  kuwa eneo hilo limekuwa likijaa na kukauka mara kwa mara katika kipindi cha miaka ya 1990 hadi 1997 huku baadhi ya wananchi wakifanya makazi katika eneo hilo kutokana na kupungua na kukauka kwa maji  na wengine kwa kuuziwa kama viwanja vya makazi bila kujua historia ya eneo hilo

Ameendelea kusema eneo hilo limekuwa likitumika kwa kilimo cha bustani  na ufugaji kwa kipindi cha mda mrefu  huku akiitaka Serikali ione namna ya kuwasaidia Wananchi ambao ni wahanga na waathirika wa eneo hilo kwa kuwasaidia kupata viwanja vingine

Mmoja wa wahanga na mkazi wa eneo hilo Ndugu. Steven Mgalu amempongeza Mkuu wa wilaya kufika katika eneo hilo  na kuonana na wahanga wa bwawa hilo na kuitaka Serikali kuandaa mkakati wa kuwasaidia wananchi wa eneo hilo kuepukana na athari za bwawa hilo

Bwawa la Katubuka lipo katika Kata ya Katubuka lililopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji likikadiriwa kuwa na  Viwanja hamsini na nne (54) huku baadhi ya wakazi wa jirani na eneo hilo wakisema katika kipindi cha miaka ya 1989s  eneo hilo lilikuwa likijaa maji na kulazimika wakazi na wanachi kutumia mitubwi kuvuka kwenda upande mwingine 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa