• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Mradi wa Billion 19.64 wazinduliwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Project

Posted on: June 4th, 2020

Na mwandishi wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Suleimani Jafo leo june 4, amefanya uzinduzi wa barabara nane(8)  zenye urefu wa Km 12.032 zilizojengwa kwa gharama ya Bilion 19.64 kwa ufadhili wa Benki ya Dunia (WB) chini ya Mradi wa Uendelezaji wa Miji na Majiji Kimkakati Tanzania(TSCP)

Kabla ya uzinduzi huo ametembelea barabara hizo nane na mifereji ya maji ya mvua iliyojengwa katika mradi huo  yenye urefu wa Km 2.35 mfereji wa Katonyanga na mfereji wa Mlole

Waziri huyo ameongea na wananchi katika eneo la Mwembetogwa ambapo ndipo jiwe la uzinduzi wa mradi huo limewekwa kando ya barabara iliyojengwa ya Mwembetogwa-Kitambwe hadi Mwanga

Akiwahutubia wananchi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji amesema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dr. John Pombe Magufuli imejipambanua katika kuwatumikia wananchi na kuhakikisha maendeleo yanapatikana

Amesema Serikali ilipokea zaidi ya Billion mia nane(800) kutoka Benki ya Dunia(WB) ambapo ilielekeza katika Halmashauri nane(8) ili  kukuzaji  miji na Majiji, ambapo Manispaa ya Kigoma/ujiji nayo ilipokea fedha za ujenzi wa miradi hiyo ya barabara, mifereji ya Maji, ujenzi na ununuzi wa mitambo ya uendeshaji wa Dampo

Waziri Jafo ameendelea kusema “watu wa Kigoma nimeridhika na ujenzi wa barabara hizi, mmesimamia vizuri na miradi hii iko chini yangu, hivyo niwambie barabara hizi mnazoziona ni maelekezo ya Mhe. Rais na amenituma nihakikishe kuona barabara hizi zinakuwa katika viwango vinavyotakiwa , hivyo niwambie kiukweli nimeridhika na miradi hiyo na niwatake muweze kuitunza”

Waziri huyo amehitimisha kwa kuwataka wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kuendelea kuchukua hatua stahiki za kujikinga na ugonjwa wa #covid-19 kwa kupiga nyungu mara kwa mara na kuendelea Kumuomba Mungu huku akisema hata Watarii nao wanaoingia  Nchini wanapiga nyungu kama sehemu ya utalii na kujikinga na ugonjwa huo

Naye Mkuu wa Mkoa Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga amewataka wakazi wa  Manispaa hiyo kutunza barabara hizo na kuhakikisha wanaboresha makazi yao ya kuishi kwa kuboresha nyumba zao hasa wale waliopitiwa na barabara katika makazi yao

Akisoma taarifa ya mradi huo Mhandisi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Eng. Wilfred Shimba amesema katika ujenzi wa mradi huo Kiasi cha Tsh Billion 1.10 kilibaki(Saving) na kuongeza kazi za ujenzi wa  vipande vya barabara vyenye  Km 0.75 ambavyo vinaingia katika barabara kuu

Mhandisi huyo amesema Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni moja kati ya Halmashauri nane(8) zinazotekeleza mradi wa Serikali ya Tanzania kupitia mkopo wa Benki ya Dunia, ambapo Halmashauri zingine ni Majiji ya Arusha, Tanga, Mwanza, Mbeya,Dodoma na Manispaa za Ilemela, Mtwara Mikindani na Kigoma/Ujiji

Mhandisi huyo amehitimisha kwa kusema Manispaa ya Kigoma/Ujiji kupitia wataalamu wake kwa kushirikiana na Wananchi watahakikisha wanasimamia miundombinu ili kuitunza na kutoharibiwa na watu wenye nia ovu

Barabara zilizojengwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni Barabara ya Kaaya-Simu, Mwanga-Kitambwe-Mwembetogwa, Barabara ya Kakolwa, Ujenzi-Nazarethi, Kagashe, Wafipa-Kagera, Maweni-Burega na barabara ya kuingia Hospitali ya Mkoa (Hospitali ya Maweni kwa Kiwango cha Lami, Ujenzi wa mifereji ya mvua ya Mlole na Katonyanga pia ujenzi wa miundombinu ya kutupia taka(skip pads)

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa