• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Mradi wa USAID Kizazi kipya wapongezwa Mkoani Kigoma, organisations

Posted on: August 19th, 2021

Na Mwandishi wetu

Mradi wa USAID Kizazi kipya  Jana August 18, 2021 ulipongezwa na wadau mbalimbali ikiwemo wanufaika wa mradi huo  Mkoani Kigoma  

Pongezi hizo zilitolewa katika tukio la Kufunga mradi wa USAID kizazi kipya kwa ngazi ya Mkoa lililofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Sunset iliyopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji


Mgeni Rasmi katika tukio hilo Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Dr. Godfrey Smart aliishukuru taasisi ya  BAKAIDS kwa kusimamia mradi huo wa Kizazi kipya kwa kutoa huduma za Afya na UKIMWI, ulinzi na Usalama wa Mtoto na ukuzaji wa kaya Kiuchumi


Pia Mgeni Rasmi aliwapongeza wafadhili wa Mradi huo kwa kutoa fedha zao katika kuboresha na kukuimarisha nyanja mbalimbali za Maisha ya wakazi wa Mkoa wa Kigoma huku akiwataka kushirikiana na Serikali katika Kuimarisha elimu ya Lishe na Kutokomeza ugonjwa wa Malaria  Mkoani hapo


Akitoa taarifa ya shughuli zilizotekelezwa na mradi kwa kipindi cha Miaka minne (2018-2021) Afisa Afya na Ukimwi  BAKAIDS Ndugu. Hamisi Karisha alisema  mradi umekuwa ukiwafikia watoto na wazazi wanaoishi na  Ukimwi , kupunguza umasikini miongoni mwa Wahitaji na kuongeza uelewa juu ya haki za watoto na kupinga ukatili wa Kijinsia

Alisema kwa Mkoa wa Kigoma awali Mradi wa USAID Kizazi kipya ulifadhiliwa kwa Halmashauri ya Kibondo, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, na baadae Halmashauri ya Kibondo kuondolewa katika mradi huo


Akitoa takwimu alisema mradi Umefanikiwa kuwafikia Wanufaika elfu saba mia nane ishirini na mbili (7,822) kwa Halmashauri ya mbili ambapo Bima ya afya kwa kaya elfu moja mia tatu hamsini na moja (1,351) na kuwafikia walengwa elfu nne mia tatu themanini na nane (4,388), mafunzo ya ufundi stadi yakitolewa kwa vijana watano (05) na wanafunzi mia mbili kumi na sita (216) wakipatiwa vifaa vya shule  


Diwani wa Kata ya Kitongoni Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Himidi Omary alipongeza mradi wa USAID Kizazi kipya kwa namna walivyokuza uchumi kwa kutoa fedha na vifaa vya kazi kwa vijana na makundi mbalimbali ya waathirika wa Virusi vya Ukimwi na kusema wao kama wawakilishi wa wananchi watahakikisha wanafatilia maendeleo ya walionufaika na mradi huo


Diwani  huyo aliwataka viongozi wa BAKAIDS kusajiri vikundi walivyokuwa wakihudumia ngazi ya Halmashauri ili vipate sifa ya kuhudumiwa Mikopo ya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu  ambapo Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilikuwa na vikundi  vya wajasiriamali

Thelathini na saba (37) vikiwa na wanachama mia nne thelathini na tisa (439) na Uvinza wakiwa na vikundi 10 vyenye wanachama mia mbili kumi na tisa (219) katika mradi wa USAID Kizazi kipya


Mmoja wa wanufaika wa Mradi wa USAID Kizazi kipya Mkazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Bi. Revina Mabuga  alisema yeye ni mwanachama katika kikundi cha wajasiriamali kilichokuwa kikifadhiriwa na mradi huo   na wao kama wanachama wameweza kupata mafunzo na semina  mbalimbali za umufamaji mashuka,  kilimo cha bustani na utengenezaji sabuni jambo ambalo limekuza uchumi wao


USAID Kizazi kipya ni mradi uliokuwa chini ya asasi ya kiraia BAKAIDS ukifadhiriwa na Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kupambana na UKIMWI (PEPFAR) na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) ambapo Nchini Tanzania ulianza rasmi mwaka 2016  



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa