• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

RAIS WA BURUNDI MHE EVARISTI NDAYISHIMIYE ASEMA "RAIS MAGUFULI KIGOMA UMEIENDELEZA SANA , BURUNDI IKIWA NA FURAHA NA KIGOMA ITAKUWA NA FURAHA ", Burundi Presdent

Posted on: September 19th, 2020

Na Mwandishi wetu

Mapema leo Septemba 19,  Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dr. John Pombe Magufuli amepokea ugeni wa  Rais wa Burundi Mhe. Evaristi Ndayishimiye Mkoani Kigoma katika Uwanja wa mpira wa Lake Tanganyika uliopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji

Katika Mapokezi hayo Rais wa Nchi ya  Burundi alikagua kikosi cha Gwalide cha Jeshi na kupigiwa mizinga ishirini na moja akiwa na mwenyeji wake Raisi wa Nchi hiyo, baadhi ya Mawaziri wa Serikali  zote mbili , Viongozi wa vyama vya kisiasa na Wananchi wa Mkoani Kigoma waliojitokeza katika Mapokezi hayo

Akihutubia Mkutano huo Rais wa Burundi amempongeza Rais wa Tanzania Mhe Dr. John Pombe Magufuli kwa namna anavyowatumikia Watanzania na kusema yeye kama kiongozi amevutiwa namna Rais huyo anavyowatumikia Watanzania huku Akisema Rais Magufuli anamchukulia kama baba yake wa Uongozi na amekuja kujifunza kwake  



Aidha Rais huyo wa Burundi amempongeza Raisi wa Tanzania kwa kuikuza Kigoma kwa ujenzi wa Miundombinu kama vile Barabara za mtaani,  Ujenzi wa Bandari ya Nchi Kavu na Ujenzi wa Mahakama huku akisema Miundo mbinu hiyo itaibadilisha Kigoma katika nyanja za kiuchumi kwa Wananchi wake

Ameendelea kumpongeza Rais Magufuli kwa jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendelea kuijenga Tanzania kwa Ujumla huku akisema Ujenzi wa Reli ya  Kisasa hautainufaisha Tanzania Tu bali pia na Nchini Burundi na Jumuia ya Afrika Mashariki kwa Usafirishaji wa Bidhaa mbalimbali

Amehitimisha kwa  kusema " Kwa sasa Nchini Burundi hali ya Usalama ni shwari , tumekaa pamoja tukaona Burundi hakuna Mtusi wala Mhutu Wote ni Warundi na tunaongea Kirundi   Na Wakoloni ndio waliotugawa  tu na hatutaki kurudia machafuko kama yale ya zamani Maana tunajua Burundi ikiwa na Furaha na Kigoma inafuraha maana tuliwasumbua kwa wakimbizi"  

Naye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dr. John Pombe Magufuli akimkaribisha Raisi huyo Wa Burundi amesema uhusiano wa kibiashara kwa Nchi hizo mbili umekuwa kutoka Tsh billion 115.15 mwaka 2016 hadi hivi sasa kufikia Tsh  billion 201

Ameendelea kusema uhusiano umeendelea kukua ambapo wawekezaji na wafanyabiashara wameendelea kushirikiana ambapo zaidi ya Kampuni kumi za Watanzania zinaendelea na Biashara katika Nchi ya Burundi

Amesema asilimia tisini na tano (95%) bidhaa za Burundi zinapita katika bandari ya Dar es salaam na kwa mwaka 2019 Tani 481,000  zilisafirishwa kwenda Nchini Burundi kupitia bandari hiyo

Raisi Magufuli ameeleza mambo watakayoyazungumza na Rais huyo wa Burundi   ikiwa ni kuendelea kuboresha Mazingira ya kibiashara baina ya Nchi hizo huku akisema watajadiliana  Madini na dhahabu za Burundi kuja kuuziwa Mkoani Kigoma ikiwa ni eneo la soko la bidhaa hizo

Ujenzi wa mtambo wa kuchenjua Madini baina ya Nchi hizo mbili, na safari za Anga zikiwa sehemu ya Mazungumzo ambapo mpango wa Ndege zinazotua Mkoani Kigoma kwenda hadi Mji wa Bunjumbula Nchini Burundi  

Aidha Rais Magufuli amehitimisha kwa kuweka wazi mpango wa Ujenzi wa Meli mpya mbili, Mkoani Kigoma zitakazotumika Katika Ziwa Tanganyika  moja itakayokuwa na uwezo wa kusafirisha abilia zaidi ya mia sita na meli moja ya Mizigo, huku meli zingine mbili ikiwemo Mv Liemba kukarabatiwa ili kukuza Sekta ya Biashara baina ya Nchi hizo na kuendelea kupanua uwanja wa Ndege ulilopo Mkoani hapo

Katika ziara ya Raisi wa Burundi, Rais Magufuli amezindua Jengo la Mahakama Kuu ya Tanzania lililojengwa Mkoani Kigoma kwa fedha za ndania mbapo litasaidia kupunguza Usumbufu na gharama kwa Wakazi wa Mkoa huo ambapo awali Wakazi wa Mkoa huo walikuwa wakisafiri kwenda Mkoani Tabora Aidha Rais wa Burundi Mhe Evaristi Ndayishimiye amefanya ziara hiyo Nchini Tanzania ikiwa ni ziara yake ya Kwanza Tangu Kuchaguliwa Nchini kwake,  Huku akisisitiza kuwa lengo la ziara yake hiyo ni kuja kujifunza namna Rais Magufuli anavyofanya kazi  na Kuwatumikia Watanzania ili imsaidie na yeye katika kipindi chake cha Utawala

PICHA NA MATUKIO ZAIDI TEMBELEA www.kigomaujijimc.go.tz





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa