• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

Posted on: May 28th, 2025

Jumla ya kaya 503,762 zinatarajiwa kunufaika na mpango wa ugawaji wa vyandarua 1,775,359 vilivyotolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ikiwa ni utekelezaji Mpango wa Taifa wa kudhibiti Maralia (NMCP) ambapo  Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa yenye kiwango kikubwa cha maambukizi.


Akizindua rasmi zoezi la ugawaji wa vyandarua hivyo kupitia hafla fupi iliyofanyika katika Zahanati

ya Mtaa wa Rusimbi Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema  kwa mujibu wa taarifa zinazotolewa kupitia mfumo wa kutolea taarifa za wagonjwa (TDHS), kwa mwaka 2024 jumla ya wagonjwa 309,080 walibainika na maambukizi ya ugonjwa huo kimkoa, ambapo idadi ya vifo ilikuwa watu  264 vikihusisha watoto 177 na watu wazima 87.


Amesema vyandarua hivyo vinatolewa bure na serikali hivyo wasimamizi wanapaswa kusimamia vizuri zoezi la ugawaji  ili viwafikie walengwa huku akitoa wito kwa wanufaika kufanya matumizi sahihi ili viweze kuleta tija katika kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa maralia mkoani Kigoma na nchini kwa ujumla.


Aidha amewataka  walengwa ambao watanufaika na mpango huo katika halmashauri zote nane za mkoa, kuvitumia vyandarua hivyo kwa usahihi na kuachana na dhana potofu kuwa matumizi yake yanaweza kuchangia kupunguza nguvu za kiume au kusababisha changamoto za uzazi kwa wanawake.


Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema zoezi la ugawaji wa vyandarua hivyo litazigusa kaya zote ndani ya mkoa wa Kigoma.


Amesema wakazi  wameendelea kuwa mashuhuda kwa ⁰kujionea namna serikali ya awamu ya sita inavyoendelea kuwagusa wananchi kupitia uboreshaji mkubwa katika utoaji wa huduma za Afya nchini.


Victor Sungusia, Afisa Ugavi MSD  amewataka wananchi kutumia vyandarua hivyo kwa lengo la kujikinga na maralia ili kutumia muda wao katika kufanya kazi za maendeleo badala ya kushinda wakishuhulikia changamoto za kiafya zitokanazo na maradhi hayo.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa