• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

SHEREHE YA MIAKA 43 YA CCM FUNZO KWA VYAMA VINGINE VYA KISIASA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, CCM celebration

Posted on: February 6th, 2020

Na Mwandishi wetu

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji wamehitimisha sherehe za kuazimisha miaka arobaini na tatu ya chama hicho kwa kushiriki shughuli za ujenzi wa vyumba vya madarasa tisa (9) unaoendelea katika sekondari ya Gungu iliyopo katika halmashauri hiyo

Wanachama hao wamewasili katika eneo hilo la Shule mapema asubuhi ya leo  Wanaume kwa Wanawake wakiwa  wamevalia sare zao za Chama huku baadhi  wakiwa na vifaa vya Ujenzi, wengine wakija kushiriki katika kusogeza tofali na mawe kwa mafundi wanaoendelea na ujenzi huo

Akiwa katika eneo la kazi Mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya Ndugu. Alhaji Yasini Mtalikwa amesema katika kuhitimisha sherehe za miaka 43 ya kuanzishwa kwa Chama Cha Mapinduzi wanachama na viongozi wa chama hicho wameamua  kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika zoezi la ujenzi wa vyumba vya madarasa 38 unaoendelea katika Halmashauri hiyo

Ameendelea kusema Chama Cha Mapinduzi (CCM)  wajibu wake ni kusimamia Serikali na kuhakikisha miradi ya Maendeleo inasonga mbele na kuinufaisha jamii inayoizunguka , huku miradi hiyo ikiwa katika hali ya ubora na viwango vinavyositahili

Amesema “  Chama na Wanachama lazima nao waunge juhudi za viongozi wa serikali kwa hali na mali ili kuhakikisha Ilani ya Chama Tawala inatekelezwa kwa maslahi ya wananchi wa Kigoma/Ujiji na Tanzania kwa Ujumla”

Amehitimisha kwa kusema zoezi hili liliofanyika leo katika kushiriki Ujenzi wa vyumba vya madarasa ni mwendelezo wa kushiriki shughuli zingine za kijamii katika idara na taasisi za Serikali na zisizo za Serikali ikionesha ni namna gani Chama na Serikali inafanya kazi pamoja ili kuifikia malengo ya Taifa

Naye mwenyekiti wa mtaa wa Masanga ambapo shule hiyo ipo Mhe. Charles William amewapongeza Wanachama wa Chama hicho kwa kushiriki ujenzi wa shule hiyo unaoendelea na kusema ujenzi huo  ulatela tija kwa jamii na kuhakikisha unamaliza tatizo la uwepo wa watoto  mtaani kutokana na uwepo wa miundombinu mashuleni ikiwa ni fursa kwa vijana kufikia malengo yao kupitia elimu watakayoipata

Ameendelea kusema katika kuhakikisha madarasa hayo yanajengwa na kukamilika wakaazi wa Kata ya Gungu wameazimia kila kaya kuchangia kiasi cha fedha shilingi elfu kumi na kusema kiwango hicho kitatosha katika ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa hayo, na wanafunzi  waliokosa nafasi kwa upungufu wa vyumba vya madarasa kuanza masomo yao mapema mwezi marchi

Naye Mkuu wa Idara ya Mipango na Uchumi katika Manispaa hiyo  Ndugu. Ferdnand Filimbi  kwa niaba ya Mkurugenzi amewapongeza wanachama wa chama hicho kwa kufikia miaka 43 ya chama hicho huku akishukuru wanachama hao na viongozi wao kushiriki katika ujenzi wa madarasa hayo tisa (9) kwa shule ya sekondari Gungu

Ameendelea kusema ukosefu wa vyumba vya madarasa kwa halmashauri kwa mwaka huu imekuwa tatizo na kufanya baadhi ya wanafunzi waliofaulu kushindwa kulipoti kwa wakati na kusema tatizo hilo tayari limewekewa mikakati ya ujenzi wa madarasa mapema na kuwa mpango endelevu na kuanzia mwezi wa tano Ofisi za kata zimepewa agizo la kuwa na benki ya tofali laki moja na kuweka mikakati ya kupata kiti,  meza,na madawati kwa shule zilizopo

Naye afisa elimu wa sekondari Ndugu. Kajanja amesema hatua hiyo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa italeta hali nzuri ya ufundishaji na ujifunzaji kwa Walimu  kuwafikia Wanafunzi kwa mahitaji ya mmoja mmoja na kuboresha suala la ufaulu kwa wanafunzi hao

Ameendelea kusema kwa kawaida wanafunzi wanatakiwa kila darasa  kuwa na wanafunzi arobaini (40) na isiyozidi arobaini na tano (45) ili wanafunzi wajifunze katika mazingira salama na yenye mvuto na mwalimu kuwahudumia wanafunzi wake pasipo msongamano

Mmoja wa wanachi wa kata ya Gungu Bi. Mwamini Hamisi amesema chama cha Mapinduzi kimefanya jambo jema katika kukabiliana na changamoto  ya vyumba vya madarasa na kuboresha elimu kwa wanafunzi wanaosoma kwa shule zilizopo katika halmashauri hiyo huku akitoa wito kwa vyama vingine vya kisiasa kuiga kile kilichotendwa na chama hicho tawala.

  

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa