• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

SHERIA YA KUDHIBITI NGONO ZEMBE KUTUNGWA KIGOMA/UJIJI.municipal committe

Posted on: November 16th, 2019

Baraza la madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya  Kigoma/Ujiji jana Novemba 15, limepitisha hoja ya kutunga sheria ndogo ya kudhibiti ngono zembe kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya biashara ya ngono katika manispaa hiyo

Hoja hiyo iliyoibuliwa na diwani wa kata ya Kibirizi Mhe Yunus Rohomvya baada ya mjumbe wa kamati ya UKIMWI Mhe. Obadia Manwigi kuwasilisilisha taarifa ya robo ya nne katika  baraza hilo ambapo alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la mabinti wa eneo la Kibirizi,Bangwe, na Ujiji kila siku za jioni kwenda mjini na eneo la Community Centre maarufu kwa Bera kukusanyika eneo hilo ili waweze kukutana na wanaume kwa lengo la kujiingizia kipato

Akieendelea kutoa hoja hiyo alisema hata hivyo kuna kundi kubwa la mabinti kutoka  Nchi jirani ya  Burundi wanafanya biashara katika maeneo mbalimbali ya starehe katika manispaa hiyo, baada ya kutoa taarifa hiyo diwani huyo aliwataka madiwani wa halmashauri hiyo kuunga mkono hoja kwa kukubaliana na wazo la kutunga sheria ndogo hiyo

Aidha awali mjumbe wa kamati ya Ukimwi akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo alisema kwa kipindi ha robo ya nne kiwango cha watu kuugua magonjwa ya ngono zembe yameongezeka ukilinganisha na kipindi kilichopita ambapo wagonjwa 544 walipimwa na kukutwa na magonjwa hayo wabaume wakiwa 76 na wanawake wakiwa 468

Nao baadhi ya madiwani wakichangia hoja hiyo wamekubaliana na hoja hiyo kutokana na vitendo hivyo kukithiri katika manispaa hiyo akichangia hoja hiyo Diwani viti maalumu Mhe Stella alisema ‘vitendo hivyo ni vibaya vinavyoendelea katika mji wetu tunapaswa kutovifumbia macho kutokana na athari zinazoweza kujitokeza katika mji wetu ikiwa na kupoteza nguvu kazi za vijana wetu’

Aidha Baraza hilo limeweza kutoa pongezi kwa halmashauri ya manispaa ya kigoma/Ujiji kwa kuongeza kiwango cha ufaulu katika matokeo ya mtihani wa kitaifa wa darasa la saba kwa mwaka 2019 na kuibuka mshindi wa kwanza katika halmashauri nane za mkoa wa Kigoma

Baraza hilo limetoa vinyago kwa shule tatu zilizofanya vibaya na kuwa wa mwisho katika mtiririko wa mshindi kwa shule za halmashauri hiyo , shule zilizofanya vibaya ni pamoja na shule ya msingi Businde, shule ya msingi Mbano na shule ya msingi Benjamini Mkapa.

Mwenyekiti wa kamati ya Uchumi,Elimu na Afya Mhe. Hussein Kaliyango alisema kamati imeweka mikakati ya kuhakikisha manispaa hiyo inaendelea kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi na elimu ya Sekondari ambapo amesema kamati zote za shule zimeshaitwa na kukabidhiwa mikakati hiyo.

Akiendelea kueleza alisema mikakati hiyo ni pamoja na kila shule kuhakikisha inapata kompyuta na printa kwa ajili ya kufanya mitihani na majaribio kila mara na kuhakikisha kamati za shule zinasimamia kupungua kwa utoro kwa shule zilizopo katika manispaa hiyo.

Naye mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndugu. Mwailwa Pangani alisema kufikia mwezio Desemba manispaa hiyo itahakikisha inanua tofali laki moja na elfu sitini na tano(165,000) na kila shule iliyopo katika manispaa hiyo itapata tofali elfu ishirini na tano(25,000).

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa