• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

SIKU ZA 16 ZA KUPINGA UKATILI ZAANZA KUADHIMISHWA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, MABARAZA YA USULUHISHI MIGOGORO NGAZI YA KATA YAJENGEWA UWEZO, ward

Posted on: November 26th, 2021

Na Mwandishi Wetu

Siku kumi na sita (16) za kupinga ukatili wa Kijinsia  zimeanza  kuadhimishwa  Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kutoa elimu na kuzijengea uwezo Mabaraza ya Usuluhishi wa Migogoro ngazi ya kata kwa lengo la kupambana na vitendo vya ukatili ndani ya jamii    

Mabaraza hayo ya Usuluhishi yameanza kujengewa uwezo Juzi Novemba 25, na 26, 2021 Manispaa ya kigoma/Ujiji katika Kata Kipampa,  Buzebazeba, Rusimbi na Kata ya Majengo ambapo elimu hiyo imetolewa na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii , Maafisa wa Jeshi la Polisi dawati la  Jinsia, Wasaidizi Wa Kisheria, Viongozi wa dini  na huku mafunzo hayo yakifadhiliwa na Mradi wa BAKAID wa kupambana na kupinga ukatili wa Kijinsia unaofadhiliwa na Shirika la Norwegian Church Aid  (NCA)

Afisa Maendeleo ya Jamii  Ndugu. Jabir Majira  wakati wa kuzijengea uwezo mabaraza ya Usuluhishi ngazi ya kata 

Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya kigoma/Ujiji  Ndugu. Jabir Majira  aliyataka Mabaraza ya  usuluhishi  wa migogoro ngazi  ya kata kuendelea  kutatua changamoto za ukatili ambazo zimekuwa zikijitokeza  kwa kutoa elimu katika mikutano ya Wananchi na Maeneo mengine yenye mikusanyiko ya Watu  kupinga vya  ubakaji,  kuwatumikisha Watoto kazi ngumu, kutowapeleka watoto Shule na unyanyasaji wa kuwanyima fursa Wanawake kujiingizia kipato

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Bi.Anastasia Daudi aliyataka Baraza hayo  kuelimisha Jamii kusimamia  Malezi ya familia na  kuripoti vitendo vya ukatili vinavyojitokeza na kutoa ushirikiano katika kushughulikia vitendo hivyo kwa Uongozi na Viongozi wa Mtaa,  Kata,  Ustawi wa jamii,  Jeshi la Polisi kutokana na athari za vitendo hivyo

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Bi.Anastasia Daudi 

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia Bi.Anastasia Daudi mradi wa wa kupambana na vitendo vya ukatili wa Kijinsia kutoka BAKAID Kigoma Ndugu. Juma Bewa aliwataka Maafisa Watendaji Kata na Mtaa kuhakikisha katika vikao na Mikutano ya Wananchi elimu ya kupinga vitendo vya ukatili inatolewa kila mara na kuweka kauli mbiu ya eneo husika ya kupinga vitendo hivyo ili jamii zipate kuwa salama

Aidha alisema Shirika la BAKAID katika maadhimisho  ya Mwaka huu imepanga  kutoa elimu Manispaa Kigoma/Ujiji ya kupinga vitendo vya Ukatili  katika Mabaraza ya Usuluhishi wa  Migogoro ngazi ya kata, Mashuleni , Viongozi wa dini na kuendeleea kutoa elimu hiyo Wilayani Uvinza katika Vijiji vya Kazuramimba na Kandaga kwa kushirikiana na Wataalamu kutoka Serikalini kama vile Maafisa Maendeleo ya Jamii,  Ustawi wa Jamii na Maafisa wa dawati la Jinsia kutoka Jeshi la Polisi, Viongozi wa Kimila na Viongozi wa dini Mbalimbali

Afisa Mtendaji wa Kata ya Rusimbi aliwapongeza Shirika la BAKAID kwa kuzijengea  Uwezo, mafunzo na elimu ya kupambana na vitendo vya Ukatili Mabaraza ya Usuluhishi wa migogoro huku akisema wameendelea kupambana na vitendo na viashiria  vya ukatili  ambapo tayari kikundi cha Malezi chanya kwa Watoto  kimeundwa na tayari wameweza   Kuwarejesha kwa wazazi watoto  ambao wamekuwa wakilala Mitaani, kutatua Migogoro ya Wanandoa, na kutoa elimu kwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitumia madawa ya kulevya

Tayari maadhimisho hayo Kitaifa  yamezinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Novemba 25, 2021 katika ukumbi wa mikutano Mlimani City jijini Dar es salaam na yanatarajiwa kuhitimishwa Desemba 10, 2021 yakiwa na kauli mbiu " Ewe Mwananchi, Komesha ukatili wa Kijinsia sasa"  







Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa