Na Mwandishi Wetu
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma amewataka Wananchi na Wakazi wa Wilaya hiyo kuendeleza umoja na mshikamano wa Kiimani uliopo Nchini Tanzania.
Ameyasema hayo Leo March 24, 2025 katika Iftari iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ukumbi wa Kigoma Social Hall huku akiwataka Wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika kukuza maendeleo ya Mji.
Aidha amewataka kuendelea kuombea amani na Viongozi wa Nchi akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan.
Iftari hiyo imehudhuriwa na Shekhe wa Mkoa, Katibu Baraza la Bakwata Mkoa, Wajumbe wa Baraza la Mashekhe Bakwata Mkoa, Mwakilishi wa Shekhe wa Wilaya, Watumishi wa Ofisi ya Mkurugenzi na Waalikwa mbalimbali.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa