• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

BENKI YA DUNIA WALIDHIKA NA MIRADI ILIYOJENGWA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI , BARABARA YA RUSIMBI ITUNZENINYUMBA ZITAKARABATIWA

Posted on: July 6th, 2018

Wakazi wa manispaa ya kigoma ujiji wametakiwa kutunza mbiundombinu iliyopo na inayotarajiwa kujengwa  kwa lengo la kukuza mji .jana may 31, 2018

Wameyaongea hayo watumishi wa benki ya dunia(World Bank) walipokuwa katika ziara ya kukagua miradi waliyoifadhili ikisimamiwa na Tanzania Strategic Cities Project(TSCP),na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) ambapo wamezungukia miradi mbali mbali ikiwemo barabara ya ya lami iliyojengwa kwa kiwango cha lami, mfereji wa maji NHC Katubuka, mfereji wa Rubengela, jengo la stendi kuu ya mabasi na vyoo katika standi hiyo,na ukaguzi wa dampo la msimba,

Watumishi waliokuwa katika ziara hiyo kutoka benki ya dunia(World Bank) ni Eng.Msiyangi Muindi, Mr. Mchalo Ignas, Mwakiluma Nkundwe, na ambapo watumishi kutoka wizarani alikuwa Eng. Ezrom(kwa jina moja) pamoja na Beatrice Mchome, Mkandarasi wa miradi hiyo Eng Jovine Ndyetabula, Mkurugenzi wa Manispaa, Baadhi ya wakuu wa idara na watumishi.

Wakiwa katika ziara hiyo walitoa ushauri mbalimbali katika miundombinu waliyoikagua kama vile utunzaji wa miundombinu hiyo ikiwa ni kusafisha mitalo katika barabara, kutotupa taka ovyo kwa mitalo hiyo kwa barabara ya Rusimbi, lakini pia waliweza kutoa pongezi kwa ujenzi uliofanyika mfereji wa Rubengela kutokana na jinsi mmomonyoko uliathiri eneo la shule ya msingi hata kupelekea baadhi ya miti kukatwa pasipo uhiari, ambapo wametoa ushauri katika eneo hilo  kujengwa ukuta ili kuleta usalama kwa watoto wa shule na kupanda nyasi kwa lengo la kuboresha mazingira.

Na wakiwa katika stendi kuu ya Mabasi Masanga waliweza kujiridhisha na ujenzi unaoendelea wa jengo la ghorofa moja, ambapo jengo hilo litakuwa na ofsi ya msimamizi mkuu wa stendi,hotel, maduka, kituo cha polisi pamoja na huduma mbalimbali, wakiwa katika stendi  hiyo waliwezakukagua  ujenzi wa vyoo unaoendelea , ukaguzi wa ofsi za kukatia tiketi ambapo walimtaka mkurugenzi aanze kuruhusu kufanyia kazi kwa kuruhusu wafanyabiashara kuingia nao kwa mkataba rafiki utakao wanufaisha wafanyabiashara pamoja na halmashauri husika na walimtaka mhandisi kuweka taa mbili zilizopelea mbele ya ofsi hizo za kukatia tiketi ambapo  aliahidi kulishugulikia ndani ya siku chache.

Baada ya hapo watumishi hao walimalizia ziara yao kwa kutembelea dampo la Msimba ambapo walijiridhisha kwa miundombinu iliyojengwa kwa majengo mawawili ya walinzi , eneo la ukarabati wa magari, na eneo la kumwaga taka linaloendelea ambapo wameshauri kujenga eneo kwa uzuri na kulaza karatasi zenye ubora zitakazo dhibiti kusambaa kwa sumu ardhini ambapo inaweza kuleta madhara kwa aldhi ya wakazi wa msimba ikiwemo taasisi ya shule iliyopo jirani na dampo hilo.

Watumishi hao wamesema wananchi ambao walioathirika katika barabara ya Rusimbi ambao nyumba zao zimepata nyufa halmashauri ifanye makubaliano mazuri na watumishi hao ili waweze kuendelea kuishi kwa uzuri.

Aidha mtumishi kutokea TAMISEMI Beatrice Mchome amewashukuru watumishi kutokea Banki ya Dunia  na kusema watahakikisha yale wale walioambiwa kufanyia kazi watahakikisha wanayafanyia kazi na kusema watafatilia katika halmashauri kuhakikisha walioathirika na zoezi hilo wanarudi katika hali yao kwa uzuri.

Naye mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji amewashukuru pia wakaguzi hao  na kusema ushauri huo wataufanyia kazi kwa ushauri wa stendi kuu katika kuingia mikataba na wafanyabiashara, kuunda kamati za usafi katika ya Rusimbi kwa lengo la kukuimarisha afya za wakazi na watumiaji wa barabara hiyo na katika kupanda miti na nyasi shule ya msingi ya Kigoma.

Wakaguzi hao walimaliza ziara yao saa tisa na nusu na kuwaaga kamati nzima ya ukaguzi kwa kuendelea kusimamia miradi hiyo na kusema wao wanaendelea na ziara maeneo mengine.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa