• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAKUU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KIGOMA/UJIJI WATAKIWA KUTOA TAARIFA YA VITENDO VYA UKATILI KILA MWEZI Against violence

Posted on: July 14th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari wametakiwa kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili vinavyotokea Mashuleni kila Mwezi na kueleza hatua zilizochukuliwa kwa kila tukio na kuripoti kwa Mamlaka zinazoshughulikia vitendo hivyo ikiwemo Jeshi la Polisi na Ustawi wa jamii  

Maagizo hayo yametolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi Leo July 14, 2022 wakati akifungua Mafunzo ya Siku Saba (7) yaliyoandaliwa  na Ofisi ya Mkurugenzi wakishirikiana na UNICEF  kwa Walimu Wakuu, na Walimu Wanasihi  juu ya Malezi, Unasihi na Ulinzi wa Mtoto awapo Shuleni

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema vitendo vya ukatili vimekuwa vikitokea ndani ya jamii ikiwemo Mazingira ya Shuleni vikisababishwa na  Watu wa Karibu  wanaowazunguka Watoto na Watoto Wenyewe  jambo linaloathiri tendo la Ufundishaji na Ujifunzaji

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema " Ni lazima tukomeshe vitendo vya ukatili kwa aina zake bila kujali nani kasabibisha, hivyo niwaagize Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari katika taarifa zenu za kila Mwezi Mnazoziwasilisha hakikisha unaambatanisha na kesi za ukatili zilizopokelewa na namna zilivyoshughulikiwa kwa kila Shule "

Afisa Ustawi wa Jamii ambaye ni Mkufunzi wa Mafunzo hayo Bi.Agnes Punjila amesema katika ulinzi wa Mtoto Shuleni Mwalimu ana wajibu wa kuhakikisha Ukuaji wa Mtoto unakuwa Kimwili, Kiakili, kihisia, Kijamii na  kwa kuzingatia Watoto Wenye Mahitaji Maalumu

Aidha amewataka Walimu Wanasihi Mashuleni kutumia mbinu tofauti tofauti katika kunasihi Wanafunzi kwa lengo la kuibua na kushugulikia na matatizo ya Ukatili ikiwemo njia ya Mwalimu (Mnasihi) kuwa kitovu cha Unasihi , Mnasihi kuwa chanzo cha Unasihi na Njia Mseto

Afisa elimu ya Watu Wazima Manispaa ya Kigoma/Ujiji na Mkufunzi wa Mafunzo hayo Ndugu. Cornel Kisinga amewataka Walimu kutenga Ofisi Maalumu za Unasihi na kushughulikia ukatili Mashuleni kwa lengo la kuwafanya Wanafunzi kujiamini katika kueleza changamoto zao

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwananchi Ndugu.Maxminus Wabera ambaye ni Mshiriki wa mafunzo akizungumza mara  baada ya Ufunguzi amesema Mafunzo hayo yatawanufaisha Kujenga Mahusiano mazuri Kati ya Wanafunzi na walimu katika kutokomeza vitendo vya ukatilinna hatimaye kuinua Taaluma   na baadhi ya Wakuu wa Shule tayari watenga ofisi za Unasihi na Shule zingine utekelezaji unaendelea

Utafiti wa Taasisi ya Haki Elimu Tanzania  mwaka 2020 ulionesha kuwa asilimia themanini na tisa (89%) ya vitendo vya kupiga na maumivu ya kimwili vimekuwa vikifanyika mashuleni na utafiti huo ukieleza vitendo vingi hufanyika zaidi kwa shule za vijijini

Kwa mjibu wa Tafiti iliyofanywa na Serikali mwaka 2009 juu ya hali ya ukatili na kutolewa mwaka 2011 ilionyesha wasichana 3 kati ya 10 na Mvulana 1 kati ya 7 walifanyiwa ukatili wa Kingono na asilimia 71 ya Wavulana na asilimia 72 ya wasichana walifanyiwa ukatili wa kimwili  na utafiti huo ulibainisha kuwa asilimia sitini (60%) ya ukatili dhidi ya watoto hufanyika majumbani huku asilimia arobaini (40%)  ukifanyika mashuleni

Picha na video zaidi tembelea Maktaba ya Tovuti www.kigomaujijimc.go.tz





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa