• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WALENGWA WA TASAF MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KUNUFAIKA NA VIKUNDI VYA KUWEKA AKIBA NA KUKOPA

Posted on: December 1st, 2021

Na Mwandishi Wetu

Mafunzo ya mpango wa kuhamasisha jamii ya kuweka  akiba na kuwekeza yamefunguliwa Manispaa ya Kigoma/Uji ji kwa lengo la kuwawezesha wanufaika wa TASAF  kuwekeza kupitia taasisi za kifedha (Vikundi) ili kuinua vipato vya kaya na kuondokana na umasikini

Mafunzo hayo yamefunguliwa leo Desemba 1, 2021 katika ukumbi wa Manispaa hiyo ambapo Wataalamu mbalimbali wanapatiwa mafunzo  ya siku tano (05)  ya nadharia na vitendo  kwa lengo la kuelimisha na kuhamasisha uundaji wa vikundi vya kuweka akiba katika mitaa

Akifungua mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji  Ndugu. Frednand Filimbi  amewataka  wawezeshaji hao watakaopatiwa mafunzo kutoa elimu kwa weredi kwa walengwa wa TASAF namna na hatua ya kujiunga katika vikundi vya kuweka na kukopa  huku akiwataka kujenga ushirikiano kwa viongozi wa Kata na Mitaa na kuhakikisha wanufaika wanajiunga kwa wingi

Mmoja wa wawezeshaji  Kitaifa kutoka TASAF Makao makuu Ndugu. Geradi Adolfu  amesema  katika kipindi cha TASAF Awamu ya tatu kaya Maskini  walipata mafunzo ya Ujasiriamali na mbinu za kuunda vikundi endelevu vya kuweka akiba ambapo jumla ya Vikundi elfu ishirini na tatu mia sita kumi na nane (23,618) vyenye jumla ya wanachama laki tatu kumi na tisa mia tisa arobaini (319,940) viliundwa kwa Halmashauri sabini na nane (78)  kutoka Tanzania Bara, Unguja na Pemba na wameweza kukusanya akiba ya Shilingi Bilion 5.9 kati ya hizo billion 2.5 zimekopeshwa kwa wanachama riba nafuu

Naye Mratibu TASAF Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Izack Vyabandi amesema  kwa mwaka wa fedha  2014/2015 hadi 2020/2021 Halmashauri hiyo imeshapokea  kiasi cha fedha  jumla ya Billion kumi na moja million mia sita ishirini na tano laki nane hamsini na nne elfu mia mbili kumi na tisa (Tsh 11,625,854,219.74/=) na kuwafikia walengwa wa kaya Maskini kwa vipindi thelathini na moja (31) vya malipo

Ameendelea kusema  manispaa ya Kigoma/Ujiji ina jumla ya Kaya elfu saba mia tisa hamsini na nne (7,954) ambazo ni wanufaika wa TASAF  na inatarajia kuunda vikundi mia tano thelathini (530) vyenye idadi ya wanakukikundi kati ya kumi (10) hadi kumi na tano (15)

Aidha amesema mpango wa kunusuru kaya Maskini Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika kipindi cha TASAF awamu ya tatu  kaya elfu sita mia tisa hamsini na mbili (6,952)  zinamiliki aina mbalimbali za mifugo na kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali

Mmoja wa wawezeshaji ambaye amehudhuria mafunzo hayo ambaye ni Mtaalamu wa Kilimo Ndugu. Haruna Mtandanyi amesema  elimu watakayoipata itawawezesha kwenda kuhamasisha  uundaji wa  vikundi vya kuweka na kuwekeza  ili kuongeza kipato, fursa na kuinuka kiuchumi kwa kaya Maskini

Mpango wa kunusuru kaya Maskini Manispaa ya Kigoma/Ujiji unatekelezwa katika mitaa arobaini na tisa (49) kati ya Mitaa sitini na nane (68) sawa na asilimia sabini (70%) ya utekelezaji kwa kaya maskini



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa