• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

"WANAOKWAMISHA UJENZI WA MIRADI YA MAENDELEO NI WAHUJUMU UCHUMI" DC KIGOMA project

Posted on: May 26th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe amesema Mwananchi au kikundi chochote kinachokwamisha kujengwa kwa miradi ya Maendeleo ni  Wahujumu wa Uchumi na Watachukuliwa hatua kwa mjibu wa Sheria za Nchi

Ameyasema hayo Leo May 26, 2022 katika Mkutano wa hadhara uliofanyikia eneo la Kwizera kata ya Bangwe Manispaa ya Kigoma/Ujiji wakati akiwahutubia Wananchi wa Kata hiyo

Mkuu huyo wa Wilaya amesema wapo Viongozi wa Kisiasa ambao wanawahamasisha Wananchi  kugomea miradi inayotarajiwa kujengwa katika Manispaa hiyo  kwa maslahi binafsi  ikiwemo mradi wa Ujenzi Mwalo wa Katonga na Ujenzi wa Soko la Mwanga Kisasa  inayotarajiwa kuanza kujengwa   mapema mwezi July , 2022

Kiongozi huyo amesema watu hao hawatavumiliwa na watachukuliwa hatua za Kinidhamu kwa mjibu wa Sheria za Nchi huku akisema taarifa  za  wanaochochea migomo ya kutopisha ujenzi tayari taarifa zao zipo ofsini kwake na vyombo vya Ulinzi na usalama vinaendelea kuwabaini      

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewaambia wakazi wa Kata ya Bangwe kujengwa kwa Mwalo wa Katonga kutasaidia kuwa na soko la Uhakika la Mazao ya Uvuvi , kuwa na Miundombinu  ya kisasa ya  ukaushaji  mazao ya Uvuvi kwa nyakati zozote za hali ya hewa,  kuongezeka kwa ajira katika mwalo huo ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa mzunguko wa fedha kwa Wananchi

Amehitimisha kwa kuwataka Wananchi kujiandaa na  kuwa tayari kuhesabiwa  katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agost 23, Mwaka huu na kuendelea kutunza miundombinu ya Anwani za Makazi inayoendelea kusimikwa katika mitaa mbalimbali

Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kigoma  Raphael Msela amewataka Wananchi kujali Miradi inayotekelezwa kutokana na Manufaa yao na kuunda vikundi vya Ulinzi shirikishi ili kuepukana na Vitendo viovu visivyofaa   ndani ya jamii

Mkuu wa idara ya Mipango na Uchumi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi amesema Serikali imeendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ya  Maendeleo kupitia fedha za Serikali kuu na Mapato ya Ndani  huku akiwataka Wananchi kuilinda na kuitunza na kuendelea kuwanufaisha jamii kubwa

Mkuu huyo wa Idara amewataka wafanyabiashara  wa Soko la Mwanga na Wachuuzi wa Mwalo wa Katonga kuendelea kupisha ujenzi wa Miradi hiyo hadi  kufikia June 30, kama walivyoarifiwa  huku akisema July 1, 2022 ujenzi utakuwa ukianza katika Maeneo hayo

Awali Diwani wa Kata Mhe. Khamis Said Betse hiyo amesema  Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kupeleka fedha katika Kata hiyo kwa lengo la kutekeleza miradi  ya Maendeleo tayari Ofisi ya Kata imepokea fedha za awali kiasi cha Million sabini na tano ( Tsh 75, 000,000/=) kwa lengo la ujenzi wa Zahanati Mpya kutokana  na Zahanati iliyopo Kata hiyo kutengwa kwa ajili ya kuhudumia magonjwa mlipuko

Ameendelea kusema tayari zaidi ya Billion Moja zimetengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Tanki la Maji litakalohudumia wakazi wa Kata hiyo na Kata zingine ambao wamekuwa wakikabiliana na Changamoto za Maji  huku akisema Mamlaka ya Maji Kigoma (KUWASA ) wamelaza mabomba eneo la kiziwani ili kuwahudumia Wananchi wa eneo hilo

Aidha ameitaka kamati ya Ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya kuwachukulia hatua za kisheria wale wanaokwamisha ujenzi wa miradi ya Maendeleo katika  Manispaa hiyo

Nao baadhi ya Wananchi waliohudhuria Mkutano huo akiwemo Bi. Getruda Ezron na William Leonard wameipongeza Serikali kwa Miradi inayoendelea kutekelezwa huku Wakisema kujengwa kwa Mwalo wa Katonga kutainua uchumi wa Wananchi na kupandisha thamani ya ardhi ya Kata ya Bangwe      






Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa