• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WANAUME NA WANAWAKE WASHAURIWA KUVUNJA UKIMYA KWA VITENDO VYA UKATILI KATIKA YA NDOA ZAO marriage

Posted on: November 29th, 2021

Manispaa ya Kigoma/Ujiji imeendelea kuadhimisha siku kumi na sita (16) za kupinga ukatili wa Kinjisia kwa kutoa elimu kwa vikundi vya wajasiriamali ikiwemo Wanawake na Vijana    

Siku ya Ijumaa Novemba 26, 2021 Maafisa Maendeleo ya Jamii wakiambatana na Wataalamu kutoka Ofisi ya BAKAID-Kigoma  chini ya Ufadhili wa Shirika la Norwegian Church Aid (NCA).  walitembelea na kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili katika  kikundi cha Wajasiriamali Wanawake kilichopo kata ya Kasimbu  (kikundi cha Huruma) wanaojishughilisha na  Ushonaji shuka, Kilimo cha Bustani , Utengenezaji wa Sabuni za Maji na Miche  

Wanachama wa Kikundi hicho walitakiwa kutovumilia na kuficha vitendo vya ukatili vinavyofanyika kwenye ndoa na familia , na kutoa taarifa katika vyombo vya kupinga unyanyasaji huo kama vile Dawati la Jinsia jeshi la Polisi, Ofisi za Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Jamii, Ofisi ya Mtendaji Kata na Mtaa ili kuepukana na athari za vitendo hivyo kama vile vifo, udhalilishaji na chuki

Afisa Maendeleo ya Jamii  Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Majira Jabir akifafanua aina za ukatili alisema Upo ukatili wa kihisia kama kuwatukana Watu  kwa maneno ya udhalilishaji , ukatili wa Kibaguzi ambapo baadhi ya watoto katika familia hupewa kazi kubwa na nyingi ukilinganisha na umri wao, ukatili wa vipigo, na ukatili wa Kiuchumi ambapo Mwanaume au mwanamke humkataza mmoja wapo kujishughulisha uzalishaji mali pasipo sababu yeyote

Mwanasheria na Wakili  kutoka Shirika la Norwegian Church Aid (NCA) Bi. Rosalia Ntirihungwa  alisema ni kosa kisheria kwa watoto wadogo chini ya Umri wa Miaka kumi na nane (18) kuingizwa na kulazimishwa kuoa au kuolewa kwa Lengo la kujipatia kipato kwa wazazi au walezi

Aidha aliendelea kuwataka wazazi na walezi kuendelea kuimalisha ulinzi kwa watoto na kuhakikisha wanapata Mahitaji Mhimu ikiwa ni pamoja  kuwapeleka shule kwa  lengo la kujipatia elimu

Afisa Mradi wa kupambana na vitendo vya ukatili wa Kijinsia kutoka BAKAID Kigoma Ndugu. Juma Bewa alisema elimu hiyo itaendelea kutolewa kwa makundi mbalimbali kwa lengo la kutokomeza vitendo hivyo vya ukatili katika Manispaa hiyo

Elimu ya kupambana na vitendo vya ukatili imeendelea kutolewa Leo Novemba 29, 2021 kwa makundi  mbalimbali kama vile Madereva boda boda na  tax katika Kata ya Gungu na Kibirizi, na kwa Mwaka huu maadhimisho haya Kitaifa yana  kauli mbiu " Ewe Mwananchi, Komesha ukatili wa Kijinsia sasa"  









Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa