• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA MKOA WA KIGOMA “WATOTO WAMEFUNGA SHULE ILI WAKAE MAJUMBANI NA SIO KUTEMBEA MASOKONI, NAAGIZA WAKAMATWE NA WAZAZI WAO WALIPE FAINI” COVID-19

Posted on: March 30th, 2020

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa  wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga leo March 30, amekemea suala la wazazi kuwachia huru watoto kutembea  ovyo masokoni na mtaani baada ya kufunga shule ili kujikinga na ugonjwa wa Corona huku akiagiza watoto hao kukamatwa na wazazi wao kulipishwa faini

Ameyasema hayo katika ziara aliyoifanya  Manispaa ya Kigoma/Ujiji ya  kutembelea maeneo yenye mikusanyiko ya watu sokoni na katika hoteli ili kujiridhisha hatua zilizochukuliwa ili kujikinga na ugonjwa huo wa Corona kwa wakazi wa Manispaa hiyo

Akiwa katika soko la Buzebazeba amesema “tumefunga shule ili wanafunzi waweze kutulia majumbani ili kujikinga na Ugonjwa wa Corona sasa imekuwa fursa ya watoto hao kutembea ovyo Masokoni, na kutumwa na wazazi wao kwa lengo la kufanya biashara , Nasema Jambo hili halikubariki lazima wazazi tuwachukulie hatua kali”

Katika ziara hiyo  Mkuu huyo wa Mkoa ametoa agizo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kufanya oparesheni ya kuwakamata watoto  wanaotembea ovyo masokoni  ili kuweza kuwafanyia mahojiano kwa lengo la wazazi wao kutozwa faini au kufikishwa katika vyombo vya kisheria

Aidha mkuu huyo wa Mkoa amewataka wafanya biashara  kuweka utaratibu mzuri kutoweka msongamano katika kila duka au bidhaa bali kuwe na mda wa kupeana nafasi kati ya mteja na mteja ili kuweza kujilinda na virusi vya Corona  vinavyoweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kugusana

Amewataka wanunuzi wa bidhaa masokoni kutohemea kila mara bali wanunue chakula na mahitaji mengi zaidi kwa lengo la kujiepusha na mikusanyiko isiyo ya lazima na kuhakikisha kunawa kila wanapotaka kuingia katika masoko

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa agizo masoko yote ya halmashauri kufungwa kwa mabomba ya maji ili maji kupatikana mda wote kwa lengo la kuendeleza usafi wa kunawa mikono kila mara ili kujikinga na ugonjwa huo

Naye mganga mkuu wa Mkoa Dr. Chacha  ametoa ushauri kwa wameliki wa hoteli kuhakikisha wanajiridhisha na wageni wanaokuwa wanaingia kupata huduma na kufuata taratibu zote za kuwahakiki ikiwepo usajili wa wageni hao na kutoa taarifa pale mtu anapoonesha dalili tofauti tofauti za Ugonjwa wa Corona’

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu Mwailwa Pangani amesema tayari elimu imeshatolewa kwa wananchi kupitia makundi mbalimbali na taasisi za serikali na zisizo za serikali katika kuhakikisha wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wanakuwa tayari kupambana na ugonjwa wa Corona

Naye mwenyekiti wa wafanya biashara  Soko la Buzebazeba Ndugu. Amrani Abduli ameipongeza Ofisi ya mkuu wa Mkoa kwa kutembelea masoko na kusema elimu ya kujikinga na Ugonjwa wa Corona tayari wameshaipata kupitia wataalamu kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji hatua na njia za kujikinga na ugonjwa huo

Katika ziara iliyofanyika mkuu wa mkoa amekataza mikusanyiko ambapo maeneo yaliyotembelea ni soko la Buzebazeba, soko la Mwanga, Soko la dagaa Kibirizi, Lake Tanganyika Hotel, Green view Hotel, Hill top Hoteli na eneo la Bangwe Beach

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa