• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAZIRI WA TAMISEMI SULEMANI JAPHO APONGEZA UJENZI WA KITUO CHA BIASHARA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI, AAHIDI KUWAFIKISHA VIONGOZI WA TRA KIGOMA KWA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO KWA KUSHINDWA KUFANYA KAZI NA KITUO HICHO. CONGRATULATIONS FROM MINISTER

Posted on: January 4th, 2019

Waziri wa TAMISEMI Sulemani Japho leo January 4, ameanza ziara yake mkoani Kigoma katika halmashauri ya Kigoma/Ujiji kwa kukagua  kituo cha biashara na  barabara zinazoendelea kujengwa na zilizokamilika.

Katika ziara yake iliyoanzia katika barabara ya kakolwa inayojengwa na Tanzania  Strategic Cities Project (TSCP) kwa ufadhili wa benki ya dunia (WB)kwa kukagua jinsi  inavyoendelea kujengwa na kuridhika na ujenzi huo na baada ya hapo msafara wa Waziri huo ulielekea katika kituo cha biashara kilichopo katika halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Akitoa taarifa kaimu  Afisa Biashara Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndg. Festo Nashoni amesema kituo kilikamilika ujenzi tangu mwezi wa 6,2018 kwa gharama ya shilingi za Kitanzania milioni hamsini na tatu laki tisa sabini na sita na mia nne( Tsh 53976400) ambapo ameeleza watu wanaopaswa kufanyia katika jengo hilo ni Afisa TRA Kigoma, Afisa biashara Manispaa ya Kigoma Ujiji, Afisa biashara halmashauri ya wilaya ya Kigoma, Afisa kutoka Uhamiaji na mawakala wa benki.

Ameendelea kusema licha ya jengo kukamilika na wao kufanya kazi katika jengo hilo tayari wameshawataarifu kwa barua wadau wote kwa lengo la kuja kufanya kazi lakini bado hakuna ambaye tayaria ameshafika kuja kufanyia kazi katika eneo hilo jambo linalosababibisha wafanyabishara kutumia gharama kubwa na mda mwingi katika kukamilisha shughuli zao katika ofsi hizo zinazotegemeana kiutendaji.

Naye waziri huyo waTAMISEMI Sulemani Japho  akiwa katika kituo hicho amepongeza halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kukamilisha ujenzi wa kituo hicho licha ya kutilia shaka gharama zilizotumika katika ujenzi wa jengo hilo.

Ameendelea kuwatia moyo watumishi wa ofsi ya biashara Manispaa ya Kigoma/Ujiji kufanya kazi kwa uzuri kwa kuhakikisha mapato ya serikali hayapotei na kuahidi kuwasilisha suala la TRA Kigoma kwa Waziri wa fedha na mipango  kushindwa kupeleka watumishi katika jengo hilo jambo linalosababisha kudolola kwa shughuli za lengo la ujenzi wa kituo hicho.

Waziri huyo amemtaka Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kuhakikisha watumishi waliopo katika halmashauri yake ambao hawajaenda kufanyia kazi katika kituo hicho wahakikishe wanaanza kazi mara moja na kumtaka kuhakikisha kituo kinafanya kazi katika hali ya uzuri.

Baada ya hapo waziri huyo alihitimisha ziara yake kwa kukagua barabara ya Rusimbi ambayo tayari imeshakamilika  na kukagua barabara ya Ujiji-Kagera ambapo amelizishwa na ujenzi unaoendelea.

Waziri huyo yupo ziarani Mkoani Kigoma kwa siku nne ambapo atatembelea miradi mbalimbali mkoani humo katika wilaya ya Buhigwe, Kasulu na Kakonko ambapo atetembelea kituo cha biashara pia.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa