• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

ANWANI ZA MAKAZI ZINAVYOWANUFAISHA WANANCHI KIUCHUMI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI Postcode

Posted on: May 13th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Zoezi la Anwani za Makazi Manispaa ya Kigoma ilizinduliwa Mapema February 09, 2022 na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Ndugu. Thobias Adengenye ambapo zoezi hilo liliendelea kwa hatua mbalimbali za utekelezaji

Mara baada ya  Uzinduzi huo makundi ya Wataalamu na viongozi wa Kisiasa walipewa elimu na  mafunzo namna zoezi hilo litakavyofanyika na kuwanufaisha wakazi wa Manispaa hiyo na Watanzania Wote

Makundi yaliyopatiwa elimu kwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigoma, Waheshimiwa Madiwani, Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi mbalimbali, Wakuu wa idara na  Vitengo, Watendaji Kata na Mitaa, Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za Mitaa, Makundi ya wajasiriamali, Wataalamu wa Ukusanyaji Taarifa   na Wananchi wote kupitia vyombo vya habari vilivyopo katika Manispaa hiyo

Zoezi la Anwani za makazi linaloendelea linahusisha   uchukuaji taarifa, Utambuzi na uwekaji wa Anwani za makazi ambapo unafanyika kwa kutoa namba ya anwani (namba ya jengo, au kiwanja),  majina ya barabara au kitongoji  na postikodi

Aidha katika zoezi hilo anwani za makazi, taasisi, na Maeneo ya Umma zaidi ya elfu arobaini na saba (47,000) zimetambuliwa na Wataalamu waliopata mafunzo na kutoa ajira ya moja kwa moja kwa  vijana  zaidi ya mia moja na ishirini (120) katika ukusanyaji taarifa na uandishi wa namba 

Aidha makundi mbalimbali ya Wajasiriamali na mafundi wa kuchomelea wanaendelea na shughuli ya uzalishaji wa namba za Anwani ambapo hadi sasa Kikundi cha vijana Talanta kilichopo Kata ya Buzebazeba eneo la Burega na makundi mengine ya Wajasiriamali wanaendelea na uzalishaji huku zaidi ya namba za Anwani Mia saba (700) tayari zimesambazwa katika Ofisi za Kata na Mitaa na kiasi cha fedha Million kumi na tatu (Tsh 13, 000,000) kinatarajia kitumika katika zoezi hilo  

Katika Mitaa sitini na nane (68)  iliyopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji zaidi ya vijana mia mbili  (200) wanatarajia kunufaika na ajira za ubandikaji wa vibao katika makazi, taasisi na maeneo ya umma kutokana na ajira ambazo Watendaji wa Mitaa hiyo watazitoa kwa wakazi husika

Kazi nyingine inayoendelea kwa makundi ya wajasiriamali ni uzalishaji wa nguzo na vibao vya majina ya barabara ambapo zaidi ya barabara elfu mbili mia moja tisini na saba (2197) zinatarajiwa kuwekwa miundombinu hiyo  mwanzo na mwisho mwa barabara husika na zaidi ya vijana sabini ( 70) wananufaika na uzalishaji wa miundombinu hiyo

Aidha kukamilika kwa zoezi hili kutaendelea kuwanufaisha kiuchumi  wafanyabiashara, Wamiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni kwa kufanya biashara Mtandaoni kwa kutangaza bidhaa na kuwafikisha wateja kirahisi ikiwa ni pamoja na ufikishaji wa vifurushi  

Faida zingine za kukamilika kwa anwani za makazi kutasaidia kila mtu anayeishi Nchini Tanzania kuwa na anwani halisi ya makazi, utambulisho wa watu wanaoishi katika maeneo husika, usajili wa mali, biashara, na kuboreshwa kwa usajili wa vizazi na vifo, ufikishaji wa  huduma za maendeleo kwa wananchi kulingana na mahitaji yao, Huduma za dharura, kama vile polisi, zimamoto na magari ya wagonjwa, zinaweza kutambua maeneo yenye dharura na kuyafikia kwa haraka


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa