• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

BARAZA LA MADIWANI LA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI LATOA VINYAGO KWA SHULE ZILIZOFANYA VIBAYA MITIHANI YA KITAIFA YA DARASA LA SABA NA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2018.Municipal commitee

Posted on: March 29th, 2019


Na mwandishi wetu

Baraza la madiwani la halmashuri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji kupitia Mwenyekiti (Meya) wake Mhe. Hussein Ruhava jana limetoa vinyago kwa shule zilizofanya vibaya katika matokep ya mitihani ya kitaifa ya darasa la saba na kidato cha nne kwa mwaka 2018.

Meya huyo wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji ametoa vinyago hivyo kwa shule za msingi tatu na shule za sekondari tatu baada ya baraza kupokea taarifa kutoka katika kamati ya Uchumi, Elimu na Afya kwa kueleza kuwa shule hizo ndizo zilizoburuza mkia katika matokeo ya kitaifa kwa matokeo ya Halmashauri.

shule zilizofanya vibaya na zilizo pokea vinyago ni shule ya msingi Mnarani, shule ya Msingi Ujiji na shule ya Msingi Businde na kwa shule za sekondari ikiwa ni shule ya sekondari Wakulima, shule ya Sekondari Kirugu na shule ya Sekondari Kasingirima.

Meya huyo aliendelea kusema halmashauri inayomikakati mikubwa ya kuhakikisha taaluma inakuwa na hasa kwa wanafunzi wa kike ambao imebainika wamekuwa wakifanya vibaya katika mitihani hiyo huku akisema tayari kampeni ya kuinua ufaulu wa mwanafunzi wa kike imezinduliwa tangu march 6, mwaka huu.

Aliwataka wadau mbalimbali wa elimu kuendelea kutoa elimu kwa jamii na wanafunzi umuhimu wa elimu hasa kwa watoto wa kike huku akisema halmashauri inatoa zawadi kwa shule na kwa mwanafunzi wa kike anayefanya vizuri kwa matokeo ya mitihani ya Kitaifa.

Akiwasilisha taarifa hiyo Mwenyekiti huyo wa kamati ya Uchumi,Elimu na Afya alisema halmashauri imekuwa ikitoa vinyago hivyo kwa shule zinazofanya vibaya kwa ngazi ya halmashauri kila mwaka jambo ambalo limesababisha halmashauri hiyo kuendelea kushikiria nafasi ya kwanza kwa ngazi ya Mkoa.

Aliendelea kueleza wataendelea kufanya hivyo kutoa vinyago kwa shule zitakazofanya vibaya ili shule hizo wajitahidi zaidi na kuhakikisha wanainua taaluma kwa wanafaunzi na matokeo ya mitihani ya kitaifa na hatimaye halmashauri hiyo kufanya vizuri zaidi katika ngazi ya Taifa.

Katika baraza hilo kamati zingine zilizowasilisha ni kamati ya Mipango miji, Ujenzi na Mazingira na kamati ya Ukimwi ,ambapo kamati ya Mipango miji, Ujenzi na Mazingira chini ya Mwenyekiti Maulidi Kacheche imelipendekeza uanzishwaji wa kampuni ya ujenzi itakayofanya kazi na kuwa na mitambo mbalimbali na kuweza kuingizia halmashauri kipato kutokana na fedha zitakazopatikana.

Meya wa halmashauri hiyo aliahirisha baraza hilo majira ya jioni na kusema baraza hilo litaendelea siku ya jumanne ambapo kamati ya Fedha na Uongozi ndipo itawasilisha taarifa yake.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa