• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

BURIANI RAIS MAGUFULI, KIGOMA/UJIJI WATAKUKUMBUKA, Bye Magufuli

Posted on: March 25th, 2021

Na mwandishi wetu

March 17,2021 itabaki  siku ya kihistoria katika vichwa vya Watanzania wengi wa Ndani na nje ya Nchi baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo cha Rais wa Tanzania Mhe. Dr John Pombe Magufuli

Makamu wa Rais(kabla ya kuapishwa kuwa Rais)  huyo akitangaza Kifo hicho alisema  Rais Magufuli  alifariki majira ya saa kumi na mbili jioni siku hiyo akiwa  katika hospitali ya Mzena iliyopo jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu  kwa maradhi ya moyo aliyokuwa akisumbuliwa kwa zaidi ya miaka kumi hali ambayo ilileta mshituko na simanzi kubwa kwa Watanzania  na raia wa Nchi zingine

kwa hakika Rais na Mhe. Dr John Pombe Magufuli  alikuwa ni kiongozi aliyependa maendeleo ya Watanzania wote hasa walio wachini ambapo yeye aliwaita Wanyonge hali ambayo ilimfanya kupendwa na wananchi wa ndani ya Nchi na wa Mataifa mengine kutokana na namna alivyokuwa akitatua kero na vilio vya wananchi hao  

Ni kiongozi aliyependa kuona matokeo makubwa katika utendaji kazi kwa viongozi wa Serikali na watu binafsi huku akiwa na shauku ya kuiona nchi ya Tanzania inakuwa eneo zuri la uwekezaji kwa wenyeji na wageni wa mataifa mengine hali iliyompa umaarufu dunia kote na kufikia malengo ya Milenia ya Uchumi wa kati kwa Taifa hilo

WAKAZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI NAMNA WATAKAVYOMKUMBUKA

Septemba 19, 2020 Rais  Dr. John Pombe Magufuli alipokea ugeni wa Rais wa Burundi Mhe. Evaristi Ndayishimiye Manispaa ya Kigoma/Ujiji  katika uwanja wa mpira wa Lake Tanganyika na kufungua jengo la Mahakamu Kuu ya Tanzania iliyopo katika Manispaa hiyo na kumbe bila kujua ilikuwa ziara yake ya mwisho hadi umauti unamkumba

Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji watamkumbuka Rais Dr. Magufuli kwa miradi ambayo ameianzisha na kusimamia katika kipindi cha uongozi wake pindi alipokuwa hai

Ujenzi na Ukarabati wa Mwalo wa kibirizi ni mradi ambao umetekelezwa katika kipindi cha Hayati Dr. John Pombe Magufuli ambapo jumla ya fedha za Kitanzania Million 447,292,077/= zilitumika katika ukarabati wa mwalo huo ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa majengo ya usafirishaji wa mazao ya uvuvi nje ya Nchi na majengo ya kuuzia samaki na dagaa kwa wajasiliamali wadogo,

Pia ujenzi wa machinjio ujiji na kuwa  ya kisasa unaendelea ambapo machinjio hayo yatasaidia kuongeza ubora wa nyama na kuhakikisha inafika kwa mlaji ikiwa salama na kufungua biashara ya nyama kwa Nchi jirani ambapo jumla ya fedha za Kitanzania Million 250,000,000/= zinatarajia kutumika huku tayari Serikali chini ya Hayati Rais Magufuli imeshatoa kiasi cha fedha za Kitanzania Million 184,000,000/= na ujenzi umeshaanza

Katika utekelezaji wa mradi wa Maji serikali ya awamu ya Tano ilitoa fedha za Kitanzania Million 42,000,000/= kwa ajili ya usambazaji wa maji kwa wananchi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji na wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma  ukitarajia kuzalisha lita Million 142 kwa siku na mahitaji yakiwa lita Million 123 hadi kukamilika, kwa sasa mradi huo unasambaza maji lita Million 17 kwa siku, kwa wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji na Mahitaji kwa sasa yakiwa ni lita Million 23 kwa siku hali ambayo imeleta matumaini makubwa kwa wakazi hao

Aidha Serikali ya awamu ya Tano chini ya Hayati Rais Dr.John Pombe Magufuli ilitekeleza ujenzi wa majengo ya Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Kigoma na ujenzi wa nyumba za Majaji kwa mwaka 2018/2019 ambapo kiasi cha fedha za Kitanzania Billion 8,900,649,022/= zilitumika katika ujenzi huo ambapo kukamilika kwa Mahakama hiyo  kumeongeza uwajibikaji kwa watumishi na wananchi kupata haki zao kwa wakati ukilinganisha awali walivyokuwa wakisafiri hadi mkoani Tabora

Vituo vya afya vimeongezewa ufanisi katika utendaji kazi ambapo kituo cha afya cha Gungu na Ujiji vinatoa huduma ya upasuaji  huku kituo cha afya cha Gungu jengo la upasuaji na kujifunguliwa kwa wanawake limejengwa amabapo serikali kuu ilitoa kiasi cha fedha Million 200,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo huku kaya za Manispaa hiyo 2400 walihamasishwa na kupata bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa

Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji hakika wataendelea kumkumbuka Hayati Rais Dr. John Pombe Magufuli katika maeneo mbalimbali ambapo fedha za utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa madarasa na miundombinu ya shule kwa  elimu Msingi kiasi cha fedha Billion 2,877,671,370/= zilitumika  na elimu sekondari kiasi cha fedha Million 250,959,030/= zikitumika katika ujenzi, zaidi ya madarasa 86 yamejengwa, matundu ya vyoo 125, ukamilishaji wa maabara 11, ujenzi wa mabweni na nyumba za walimu

Akifungua Bunge la 12 jijini dodoma wakati akihutubia Rais Dr. John Pombe Magufuli alitaja zao la Michikichi kuwa zao la kimkakati ambapo hadi sasa Halmashauri zote mkoani kigoma na taasisi mbalimbali zinazalisha miche ya kisasa ya  michichikichi na kuigawa kwa wananchi bure ambapo zaidi ya miche 45,000 zimeshazalishwa manispaa ya Kigoma/ujiji na kuigawa kwa wakulima na wakazi wa Manispaa hiyo bure




Hakika ni Majonzi na simanzi ambayo Rais Dr. Magufuli ameyaacha ambapo itakumbukwa katika ziara yake ya mwisho Mkoani Kigoma alisema Serikali inampango wa kujenga meli mpya mbili zitakazotumika katika ziwa Tanganyika na zikiwa na uwezo wa kubeba abiria zaidi  ya mia sita na mizigo kila moja huku ujenzi huo utaenda sambamba na ukarabati wa meli  zingine mbili ikiwemo Mv Liemba  ambapo kiongozi huyo amefariki kabla ya kufikia lengo hilo huku wakazi wa Manispaa hiyo wakiwa na imani na Rais aliyepo sasa Mhe. Samia Suluhu Hassan kuendeleza miradi hiyo

Rais Dr. John Pombe Magufuli atakumbukwa na wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji na itakuwa historia hata kwa vizazi vijavyo ikiwa ni pamoja na ujenzi na upanuzi wa uwanja wa ndege unaoendelea, ujenzi unaoendelea wa Bandari ya Nchi kavu Katosho, ujenzi wa bandari ya Ujiji na Kibirizi unaoendelea

Katika ziara iliyofanyika Nchini kwa baadhi ya mikoa ya Kuaga mwili na kutoa heshima za mwisho kwa Rais Dr. Magufuli  Simanzi zimetawala kwa Watanzania walio wengi kuondokewa na mpendwa wao huku baadhi ya watu wakipoteza fahamu kutokana na Mapenzi waliyokuwa nayo na Rais huyo wengine wakimuaga kwa kutandika mavazi na Maua kama ishara ya heshima na kumuaga, lakini ni faraja kwa wakazi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji wakiwa tayari kutoa ushirikiano kwa Rais mpya Mhe. Samia Suluhu Hassani baada ya kuapishwa katika kutekeleza na kuiendeleza miradi mbalimbali iliyopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Halmashauri zingine zote Nchini na Tanzania kwa Ujumla


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa