• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

CCM WILAYA YA KIGOMA YARIDHISHWA NA UJENZI WA VYUMBA MADARASA KIGOMA/UJIJI CCM Political party

Posted on: December 21st, 2022

Na Mwandishi Wetu

Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigoma Jana Desemba 20, 2022 walifanya ziara ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa 57 unaoendelea Manispaa ya Kigoma/Ujiji ikiwa ni ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya chama hicho

Katika ziara hiyo Viongozi na Wajumbe wa Kamati hiyo waliridhishwa na ujenzi huku wakipongeza usimamizi   wa Wataalamu  chini ya  Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo

Manispaa hiyo ilipokea kiasi cha fedha za Kitanzania Billion moja na milion mia moja arobaini na Sita (Tsh 1, 146, 000, 000/=)  kutoka Serikali  Kuu  kwa lengo la ujenzi wa vyumba hivyo vya Madarasa ikiwa ni maandalizi na mapokezi ya Wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa Mwaka 2023

Akizungumza  Katika ziara hiyo Katibu wa itikadi uenezi wa CCM Wilaya ya Kigoma  Ndugu. Haruna Kambiro aliwapongeza Wataalamu wa Manispaa hiyo kwa Usimamizi wa ujenzi  wa Madarasa kwa Shule kumi na sita (16) huku akiwataka kuendelea kukamilisha ili kuwanufaisha wanafunzi pindi Shule zitakapofunguliwa

Mjumbe wa Kamati hiyo na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Kilumbe Shabani Ng'enda alisema ujenzi wa miundombinu hiyo unaendelea kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya Madarasa katika Manispaa hiyo na kufanya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya upili kuanza kwa wakati mmoja

Mjumbe wa Kamati hiyo na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe aliwataka Wananchi kuitunza Miundombinu hiyo kwa kutoruhusu uhalibifu wowote huku akiwataka Wazazi kuhakikisha kila Mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga na masomo ya upili anaripoti kwa wakati

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Athumani Msabila alisema ujenzi wa vyumba vya Madarasa unaendelea kukamilishwa katika hatua za mwisho ili kuanza kutumika mapema mwezi Januari 2023

Alihitimisha kwa kusema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali na inatarajia kuleta fedha zingine za Maendeleo katika Ujenzi wa Miundombinu ya vyumba vya Madarasa kwa Shule za Msingi kupitia mradi wa Boost    





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa