• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

CCM YAAHIDI KUFUTA HATI CHAFU MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI.Oath

Posted on: November 28th, 2019

Na mwandishi wetu

Chama Cha Mapinduzi (CCM)  jana Novemba 28, wameahidi kufuta hati chafu katika kipindi watakachoitawala Manispaa ya Kigoma/Ujiji  kutokana na ushirikiano watakaoufanya kati ya viongozi wa serikali za mitaa na wataalamu wa halmashauri hiyo

Aliyasema  hayo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Kigoma Ndugu. Yassin Mtalikwa katika ukumbi wa manispaa hiyo katika sherehe za kuwaapisha wenyeviti wa mtaa na wajumbe waliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika Novemba 24 Nchini  wa kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa

Akihutubia wenyeviti, wajumbe wawilishi wanawake, wajumbe mchanganyiko, na waalikwa  kiongozi huyo wa chama aliwataka viongozi hao waliochaguliwa kuwatumikia wananchi kwa kutatua matatizo yaliyopo katika ngazi ya mtaa

Aliendelea kuwataka viongozi hao waliochaguliwa kufanya kazi kwa ushirikiano baina ya Chama Cha Mapinduzi, na Serikali chini ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa kutambua matatizo yaliyopo ngazi ya mtaa si ya Mwenyekiti  tu wa mtaa bali ni ya wadau wote wa maendeleo

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wa wilaya hiyo Ndugu.Kitundu alisema Manispaa ya Kigoma/Ujiji sasa inaenda kupata maendeleo kutokana na wananchi kukiamini chama hicho na kukipatia ushindi  utakaofanya viongozi hao kufanya kazi kwa ushirikiano ukilinganisha na uongozi uliopita kuwa uongozi Mseto

Aliwataka viongozi hao waliowachagua kufanya kazi kwa weledi na kuahidi kwamba viongozi hao watakuwa chachu ya maendeleo na watakuwa mfano wa kuigwa kutokana na mafunzo waliyoyopata ya kiuongozi na kuahidi barua zote za kuwapitishia wananchi zitakazopita kwa viongozi hao itakuwa zikitolewa bure

Alihitimisha kwa kusema ushindi kwa Chama Cha Mapinduzi ni hatua ya awali ya kuelekea uchaguzi  mkuu kwa mwaka 2020 na kusema tayari wakazi wa Manispaa hiyo wamekielewa chama hicho na kuahidi kupata ushindi katika uchaguzi ujao

Naye mkurugenzi wa  Manispaa hiyo Ndugu. Mwailwa Pangani aliwapongeza viongozi na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi kwa kupata ushindi wa 100% katika uchaguzi ulifanyika na kuwataka viongozi waliochaguliwa kuipatia ushirikiano katika kuhakikisha mapato ya halmashauri hiyo yanakuwa makubwa

“naomba ushirikiano wenu, na naamini kuchaguliwa kwenu itakuwa ni tiba kwa halmashauri kutokana na viongozi wote kuwa wa chama kimoja hivyo naamini mapato yatakuwa makubwa kutokana na ushirikiano mtakaouonesha ukilinganisha na uongozi uliopita” alisema Mkurugenzi huyo

Aliendelea kuwataka viongozi hao kuhakikisha wanasimamia usafi wa maeneo yao ya kiutawala wakishirikiana na watendaji wa mitaa na kata ili kuhakikisha manispaa hiyo inakuwa safi na mfano mzuri katika kujali afya za wakazi wa manispaa kutokana na ufunguzi wa dampo la kisasa uliofanyika hivi karibuni

Naye mmoja wa wenyeviti kutoka mtaa wa Mwanga Sokoni Mhe. Elia Mfaume aliwataka viongozi  kwenda kufanya kazi kwa kutatua changamoto za wananchi na kuahidi kutoa ushirikiano kwa serikali na Chama Cha Mapinduzi

Sherehe hiyo ilihitimishwa kwa kuwaapisha wenyeviti 68 na wajumbe wawikilishi wanawake 136, na wajumbe mchanganyiko 204 kwa kuapa kiapo cha uadilifu, na kiapo cha utii na uadilifu wakiapishwa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mwanzo Kigoma Bi. Mushi(kwa jina moja)

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni moja ya halmashauri iliyofanya uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 24, Chama Cha Mapinduzi kikiibuka kwa ushindi wa asilimia mia moja ambapo uchaguzi ulifanyika kwa kata 9 na kupata  wenyeviti 14 na wajumbe 45 ambapo kata 10 tayari Chama Cha Mapinduzi kilikuwa kimeshapita bila Kupingwa

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa