• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

DIAMOND PLATINUMZ AAHIDI MEZA 100 KWA WAFANYABISHARA WA KIGOMA NIGHT MARKET, ASEMA ATARUDI DAR KWA USAFIRI WA TRENI TENA , artist

Posted on: December 30th, 2019

Msanii wa Bongo fleva Nasibu Abdul  maarufu kwa jina la Diamond Platinum leo desemba 30, ameahidi kutoa meza mia moja (100) kwa wafanyabiashara wa soko la Kigoma night market kutokana na wafanyabiashara hao  bidhaa zao kuzitandaza chini pindi wanapokuwa katika soko hilo

Msanii huyo ameyasema hayo alipokutana na kamati ya ulinzi na usalama ya  Mkoa huo  ikiongozwa na katibu tawala wa mkoa huyo Ndugu. Rashidi Mchata kwa niaba ya Mkuu wa mkoa, uongozi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji na wasanii alioambatana nao msanii huyo Diamond

Akiongea katika kikao hicho msanii huyo amesema amekuja kusheherekea miaka 10 ya Mafanikio katika mziki anaoufanya na hadi sasa jamii imeupokea vizuri kutokana na vijana kujingizia kipato binafsi, kuendesha familia  na kulipa kodi mbalimbali za serikali kutokana na sanaa hiyo

Ameendelea kusema kwa sasa kuna mambo ambayo tayari ameyafanya katika mkoa wa Kigoma kama mwanzo tu  kutokana awali kutokuwa na mawasiliano ya moja kwa moja na uongozi wa serikali, na kusema tayari amejenga visima vinne (4) vya maji safi, ujenzi wa msikiti wa Azizi na madrasa na kusema ataendelea kuisaidia jamii katika ujenzi wa vyumba vya madarasa na kukuza vipaji vya sanaa kutoka kwa vijana wa mkoa huo

Msanii huyo ameipongeza Shirika la Reli Tanzania(TRC)  kwa ushirikiano waliopewa katika safari waliyoianza kutoka Mkoa wa Dar es salaam hadi kufika Kigoma na kusema ni maendeleo makubwa sana na uwekezaji unaofanyika katika shirika hilo kwa kiwango cha standard garge na kuahidi atarudi kwa treni hiyo msanii huyo akiwa na timu yake yote

Amehitimisha kwa kuwashukuru wakazi wa mkoa wa Kigoma kwa kujitokeza kwa wingi katika mapokezi aliyoyapata jana desemba 29 alipofika na kuvishukuru vyombo vya usalama kwa ulinzi ambao wameupata na ambao wanaendelea kuwataka huku akiwataka kushirikana hadi watakapokuwa wakiondoka kurejea jijini Dar es salaam

Naye katibu Tawala wa Mkoa huo Ndugu. Rashidi Mchata awali akimkaribisha katika mkoa huo amempongeza kwa kuja kusheherekea miaka kumi nyumbani akiwa katika sanaa ya mziki huo na kusema wako tayari kumpa ushirikiano katika maeneo atakayopita na matamasha  atakayoyafanya katika suala la ulinzi na usalama

Akiendelea kutoa taarifa za maendeleo ya mkoa huo amesema mkoa wa Kigoma umeendelea kuimarika katika miundondombinu  ya barabara kama vile barabara zilizozengwa manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, kuongezeka kwa hali ya ufaulu na uandikishaji  kwa wanafunzi ambapo amesema kwa mwaka 2018 uandikishaji ulipanda kwa  83% na ufaulu kwa mtihani wa kidato cha nne 2015-2019 umepanda kutoka 71% hadi 83% na ufaulu wa kidato cha sita kutoka 89% hadi 99.25%

Pia amamtaka msanii huyo kuendelea kuutangaza mkoa wa Kigoma kwa kuwakaribisha wageni kuja kuweza katika mkoa huo lakini pai kutangaza vivutio mbalimbali vilivyopo kwa kutumia kampuni ya Wasafi yenye vyombo vya habari radio na televisheni  kama vile hifadhi ya Gombe na Mahare, meli ya Liemba, majumba ya makumbusho na uhifadhi wa ziwa Tanganyika

Amehitimisha kwa kumtaka msanii huyo kuwa balozi wa Tanganyika Bussnes Summit , ambalo ni kongamano la kibaiashara linalohusisha mikoa jirani ya mkoa wa Kigoma na nchi jirani ikiwemo Burundi, Rwanda, Zambia na Congo katika kujadili namna ya ukusaji biashara na uwekezaji katika mkoa wa Kigoma.

Aidha Mbunge wa viti maalumu anayewakilisha Vijana Bungeni Mhe. Zainabu Katimba amempongeza msanii huyo kwa mafanikio aliyonayo tangu aanze sanaa ya mziki na kusema ni chachu kubwa kwa vijana wengine kujifunza kutoka kwa msanii huyo katika Nyanja za maisha mbalimbali

Ameendelea kuwataka wasanii wote na viongozi mbalimbali kuendelea kuunga mkono serikali ya awamu ya Tano kwa jitihada zinazozifanya katika kuboresha mazingira ya vijana na Watanzania wote serikali inafikia malengo yake iliyoyakusudia ili kuboresha maisha ya wananchi wote

Msanii huyo anatarajia kufanya tamasha katika uwanja wa Lake Tanganyika Usiku wa Desemba 31, ikiwa kiingilio ni Bure kwa kuwashukuru wakazi wa mkoa huo kwa kumshika mkono ndani ya miaka kumi hadi mafanikio aliyonayo na tamasha hilo linatarajiwa kuhudhuliwa na watu mbalimbali wa mkoa huo wakiwemo wageni kutoka nchi jirani Burundi, Congo na Rwanda

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa