• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

ELIMU YA KORONA YATOLEWA MAKANISANI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI , WAUMINI WAAHIDI KULIOMBEA TAIFA DHIDI YA UGONJWA HUO, COVID-19

Posted on: March 21st, 2020

Na Mwandishi wetu 

Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji imendelea kutoa elimu ya kujikinga na Ugonjwa wa Corona katika taasisi za dini huku waumini wakishukuru juu ya elimu hiyo waliyoipata

Elimu hiyo imetolewa leo March 21 katika kanisa la Waadventista wasabato Mwasenga ambapo jumla ya Waumini wakubwa sabini na sita(76) na watoto sabini na saba (77), huķu kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKT) Mlole watoto wadogo 180 wakipata elimu hiyo

Mganga na Mratibu wa Ukimwi katika Manispaa hiyo Dr.Shabaan Magorwa amewataka waumini hao kuzingatia kanuni za kujiepusha na Ugonjwa wa Corona kwa kuepuka na kuachana na utamaduni wa kusalimiana kwa mikono,  kuachana na tabia ya kukumbatiana na kubusiana kwa kipindi hiki cha ugonjwa huu

Katika semina hiyo waliyoipata wamekumbushwa kuhakikisha suala la usafi linazingatiwa, huku wakiaswa kunawa mara kwa mara kwa maji yanayotiririka na sabuni ili kuweza kupambana na virusi vya corona


Aidha mganga huyo  ameendelea kusema ugonjwa wa corona ni hatari kwa afya na kuzorotesha uchumi kutokana na namna mgonjwa aliyepata ugonjwa anavyohudumiwa  "kwa kweli ugonjwa huu unadhorotesha uchumi kutokana na gharama ya vifaa tiba, idadi ya madaktari wanaomuhudumia mgonjwa mmoja ni gharama kubwa jambo ambalo linaweza kuathiri uchumi wetu, hivyo tufate kanuni ili tuweze kuepukana na ugonjwa wa corona " Amesema Daktari huyo

Ameendelea kuwataka jamii kutoa taarifa sahihi katika mamlaka zinazohusika na kuitaka jamii kuachana na tabia za wale wanaodanganya  kuwa na ugonjwa huo na kuzua taharuki kwa wengine huku akisema anayesadikika kuwa na ugonjwa huo lazima awe na historia ya kusafiri kutoka nje ya nchi au amekutana na wageni

Ameendelea kuwataka viongozi wa Makanisa hayo kutojenga dhana potofu juu ya Ugonjwa huo ukilinganisha na wachungaji wanaoleta taharuki kwa waumini wao na kuwanywesha baadhi ya madawa ambayo sio maalumu kwa kunywa na kuhatarisha afya zao na kuwataka watumie mda wao kuliombea taifa kuhusu Ugonjwa huo

Naye Mzee wa Kanisa wa Kanisa la Waadventista wasabato Mwasenga Ndugu. Sauli Malekela ameshukuru kwa elimu hiyo iliyotolewa huku akisema wao kama viongozi wa kanisa hilo hawataleta taharuki kwa waumini wao bali kuendelea kutoa elimu kwa mjibu wa Wizara ya Afya  na kusema wao kama kanisa wameweka utaratibu wa kuweza kuombea Taifa kuepukana na athari zinazoweza kutokana ugonjwa huo na kuwaombea Watanzania sita (6) ambao tayari wamegundulika kuwa na ugonjwa huo

Nao baadhi ya waumini wa kanisa la Waadventista wasabato akiwemo Ndugu. Batholomeo Bizoba amesema elimu waliyoipata ni mhimu sana na wataifanyia kazi kwa kuzingatia kanuni za afya na wao kutoa elimu hiyo kwa watu wengine  huku wakoshukuru Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa kuwapelekea elimu hadi Makanisani

Zaidi ya wagonjwa 11,000 yatari wamekwishafariki duniani kutokana na Ugonjwa wa Corona na wagonjwa 250,000 wamepatikana na virusi vya Ugonjwa huo ambao ni ugonjwa unaoshambulia mfumo wa kupumua huku Tanzania wagonjwa 6 wamethibitishwa kuwa na ugonjwa huo pasipo kuwa na vifo


Picha zaidi ingia katika maktaba ya picha 



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa