• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI IMEPOKEA UGENI WA WABUNGE, MKUU WA WILAYA NA MADIWANI 19 KUTOKA NCHINI BURUNDI.Polical leader visitor

Posted on: June 16th, 2019

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji jana june 15, imepokea ugeni wa viongozi wa kisiasa kutoka nchini Burundi ikiwa ni kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa Jumuia ya Afrika Mashariki na kujifunza namna halmashauri inavyowahudumia wananchi kupitia miundombinu iliyoijenga.

Ugeni huo uliofika jana kutoka katika mji wa Nyanza Lake nchini Burundi ukiwa na Wabunge wawili(02), Mkuu wa Wilaya, Madiwani 19 pamoja na baadhi ya wataalamu wa mambo ya fedha ikiwa ni ziara ya siku mbili (02) katika halmashauri hiyo.

Akiwakaribisha wageni hao katika ukumbi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji  Meya wa halmashauri  hiyo Mhe. Hussein Ruhava aliwashukuru kwa kuchagua kuja kujifunza katika halmashauri hiyo kutokana na Nchi ya Tanzania kuwa na halmashauri nyingi.

Meya huyo Alisema  “viongozi ninyi  mliokuja ni viongozi wa kisiasa wenye dhamira ya kuwahudumia wananchi , kutimiza dhamira ya wananchi na kutekeleza huduma za jamii katika mahitaji ya wananchi jambo ambalo pia ni dhamira ya viongozi wa halmashauri yetu”.

Aliendelea kusema katika ziara hiyo waliyoichagua katika halmashauri hiyo wataweza kujifunza mambo mengi zaidi katika miradi watakayotembelea ikiwa baadhi ya miradi ni Nguvu ya wananchi na Miradi mingine ni kutoka serikali kuu.

Naye Barozi msaidizi katika ubarozi mdogo Mkoani Kigoma Mhe. Kabura  aliweza kushukuru kwa mapokezi  yaliyofanyika kwa viongozi kutoka nchini Burundi na kusema anaamini ziara itakuwa na tija kwa viongozi hao pamoja na wananchi wanaowaongoza katika maeneo yao ya kazi.

Baada ya ukaribisho huo katika ukumbi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ziara ilianza kwa kutembelea miradi mbalimbali pamoja na uwekezaji uliofanyika katika halmashauri hiyo ambapo jumla ya miradi 6 ilitembelewa na viongozi hao kutoka Nchi jirani ya Burundi ikiwa ni pamoja na Bandari ya Mkoa , Majengo ya madarasa mapya shule ya Msingi Kigoma,  Mwalo wa Kibirizi, Stendi mpya ya Masanga, Soko la jioni Mwanga  na forodha ya Ujiji.

Wakipewa taarifa katika Bandari ya Mkoa wa Kigoma namna inavyofanya kazi  na Kaimu meneja wa bandari hiyo Ndugu. Madiwa Muhajiri  alisema  “ kwa sasa bandari inafanya kazi nzuri na inajiendesha kwa faida katika kipindi hiki cha awamu ya tano”.

Aliendelea kusema katika bandari hiyo wanasafirisha na kupokea mizigo kutoka katika nchi ya Burundi na  nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na wanaeneo kubwa la kupakia na kushusha Mizigo, wana stoo ya kutunzia mali za wateja na usalama wa kutosha katika mizigo inayoingia na kutoka.

Aliendelea kusema kwa sasa hakuna udanganyifu wowote unaofanyika kutokana na vifaa vya kazi vilivyopo kama vile Mzani  na bandari inajikita kutengeneza meli mpya kupitia shirika la meli( merine service)

Naye kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi akitoa taarifa katika soko la jioni la Mwanga (Mwanga night market) alisema soko hilo limejengwa kupitia wafadhili wa Local Investimate Climate (LIC) wanaojishughulisha katika kuboresha mazingira ya wafanyabiashara na soko hilo linaleta matokeo mazuri katika kuwahudumia wakazi wa manispaa .

Nao baadhi ya viongozi kutoka katika mji wa Nyanza Lake nchini Burundi waliweza kuzungumzia ziara yao akiwemo Bi. Herena Senga  mtaalamu wa masuala ya Fedha na Uchumi alisema  “tumekuja ili tuone namna halmashauri hii ya manispaa ya Kigoma/Ujiji inavyowahudumia wananchi na mna rasilimali za kutosha naona ninyi mko matajiri sana ukilinganisha na tarafa yetu ya Makamba”.

Naye Naibu meya wa manispaa ya Kigoma/Ujiji akizungumzia ujio wa viongozi hao alisema “nimefurahishwa na ujio wa Viongozi hao na nimejifunza  suala la upendo kwa viongozi hao waliokuja Nchini na ziara yao imekuwa fundisho hata kwa madiwani wa halmashauri yetu”

Katika ziara iliyoanza jana june 15 ikiwa ni ziara ya siku mbili katika halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji viongozi  Wabunge hao, Mkuu wa wilaya na Madiwani wa mji wa Nyanza Lake watabadilishana na uzoefu wa kazi na namna wanavyowahudumia wananchi na  madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ikiwa ni katika kudumisha ujirani mwema na kudumisha Jumuia ya Afrika Mashariki.

PICHA ZAIDI INGIA KATIKA MAKTABA YA PICHA.

 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa