• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI YAPONGEZWA KWA KUONGEZA MAPATO YA NDANI KWA 36%.

Posted on: July 26th, 2019

Halmashauri ya manispaa ya kigoma ujiji leo july 26, imepongezwa kwa kuongeza mapato ya ndani kwa  kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Pongezi hizo zimetolewa na wageni kutoka Benki kuu na  Ofisi ya Rais-TAMISEMI walipokutana na Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri  na wakuu wa idara baada ya ziara yao ya siku nne ya kufatilia utendaji kazi na ukaguzi wa mahesabu katika miradi ya Uendelezaji miji na Majiji kimkakati Tanzania ( TSCP) unaofadhililiwa na benki ya dunia (WB).

Akiiongea katika kikao hicho Ndugu. Evans Mgeusa mhasibu wa mradi wa Uendelezaji wa Miji na Maji Kimkakati Tanzania(TSCP) kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI amewapongeza wataalamu wa halmashauri hiyo kwa kuibadilisha halamshauri hiyo kimaendeleo katika usimamizi wa miundombinu mbalimbali.

Ameendelea kusema kadri ujenzi wa miundombinu ya barabara na masoko  unavyoendelea kukua usababishe kuboreka kwa maisha ya wakazi wa manispaa hiyo jambo litakaloleta matokeo makubwa katika ongezeko la kipato cha halmashauri nakuweza kujiendesha bila shida ya aina yeyote.

Ameendelea kusema halmashauri ina wajibu wa kusimamia vyanzo vya mapato vilivyopo na kuendelea kuibua vyanzo vipya  vya mapato katika kuhakikisha halmashauri inajiendesha bila kuwa na vikwazo vya kifedha na kuweza kuboresha huduma za wananchi kama vile afya, elimu na uchumi.

Naye mtaalamu wa maswala ya fedha kutoka Benki kuu Ndugu. Nkundwe Mwakiluma katika kikao hicho ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuongeza kipato kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa 36% kutoka katika mapato halisi ya billion moja na themanini na nane elfu laki mbili sitini na saba  (Tsh 1,088,267,000/=) ukilinganisha kwa  mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo mapato halisi yalikuwa bilioni moja na sabini na nne elfu laki tano sabini na mbili mia nane sabini na nne (Tsh 1,074,572,874/=).

Ameendelea kusema katika ukaguzi uliofanyika  wa usimamizi wa masuala ya fedha katika halmshauri hiyo wamegundua mfumo wa mapato na mfumo wa epicor uko vizuri katika uendeshaji na kuwa na viwango vinavyofanana licha ya tofauti ndogo katika mambo ya kifedha suala ambalo lilikuwa na tofauti na awali.

Ameendelea kusema kwa jitihada zinazoonekana sasa halmashauri ina juhudi thabiti za kuhakikisha hati chafu inaondoka kutokana na kupatikana kwa hati chafu hiyo kwa miaka mitatu mfulululizo  “ nimeona jitihada kubwailiyofanya na Mkurugenzi wa halmashauri hii kupitia ofisi ya Mweka hazina kutaka kuondoa hati chafu iliyopo kwa vitabu ambavyo tayari vimeshafungwa na kupungua kwa hoja za ukaguzi”

Ameendelea kuwataka wataalamu kuendelea kushughulikia hoja za ukaguzi za mkaguzi wa ndani kabla ya Mkaguzi wa nje  hajazifanyia kazi na kusababisha kwenda ofisi ya CAG zikiwa tayari  zimejibiwa jambo litakaloiletea halmashauri hati iliyosafi.

Ameendelea kuitaka halmashauri kuboresha utendaji kazi wa ofisi ya Mkaguzi wa ndani kwa kuongeza watumishi katika ofisi hiyo ambapo ameipongeza pia GIZ kwa vifaa walivyovitoa katika ofisi hiyo kwa kutoa komputa nne laptop na printa moja katika kuleta ufanisi wa kazi.

Ameendelea kuipongeza ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa kuwa na kitengo kinachoratibu malalamiko ya miradi ya TSCP na malalamiko ya wananchi hali inayosababisha kuondoa migongana baina ya ofisi ya Mkurugenzi na wananchi wanao pitiwa na miradi katika makazi yao.

Naye kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndugu. Emmanuel Katemi amewashukuru wageni hao kwa ukaguzi walioufanya na kuahidi kuwa halmashauri  itaendelea kuboresha na kuibua  vyanzo vipya huku jitihada za kuondoa hati chafu zikiendelea kufanyika.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa