• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI YAPONGEZWA KWA KUTOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 170,000,000/= KWA MAKUNDI YA WAJASILIMALI.congraturations

Posted on: October 4th, 2019

Halmashauri  ya Manispaa ya manispaa ya Kigoma/Ujiji  jana Octoba 3, imetoa mikopo ya  shilingi million mia moja na sabini(170,000,000/=) kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya serikali ya awamu ya tano.

Mikopo hiyo iliyotolewa na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga  kwa vikundi 46 ikiwa ni kwa mashariti nafuu  ambapo watarejesha pasipo kuwa na riba yeyote.

Akitoa taarifa kaimu mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii wa manispaa hiyo Ndugu. Jabiri Majid alisema halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji imekuwa na utamaduni wa kuhamasisha vikundi vya wajasili amali  wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuunda vikundi vya ujasiliamali  kwa lengo la kuinua uchumi wa makundi hayo na kuweza kujipatia mikopo itakayokuza miradi yao.

Aliendelea kusema kwa sasa halmashauri imepiga hatua kubwa katika mapato ya ndani kutokana na mwaka jana kutoa mikopo  kwa makundi hayo shilingi million ishirini tu (20,000,000/=)  licha ya mikopo hiyo kuleta matokeo makubwa ya vipato kwa akina mama wanaofuma mashuka na kuuza dagaa, walemavu wanaouza vyakula na vijana wanaofanya biashara ya usafirishaji (bajaji na bodaboda).

Ameendelea kusema changamoto wanayokutana nayo ni baadhi ya vikundi vya wajasiliamali hao kutorudisha fedha hizo kwa wakati, vikundi vinavyoundwa na vijana kutaka mafanikio ya haraka na vikundi vingine kuvunjika kabla ya kurejesha na kusema kwa kipindi cha mwaka 2012 hadi 2019 milioni thelethini na tisa (39,000,000/=) hazijarejeshwa ikiwa ni wadaiwa sugu na tayari hatua ya ufatiliaji na wengine kupelekwa mahakamani imeshaanza.

Naye mjasiliamali na  mwenyekiti wa dawati la uwezeshaji kwa wanawake kiuchumi Bi. Maria Kandoga akitoa salamu kwa niaba ya vikundi vingine alisema halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji imekuwa msaada mkubwa katika kuinua uchumi wa vikundi vya wajasiliamali kupitia wataalamu wake ambapo amesema watalaamu wamekuwa wakiwatembelea na kufatilia miradi wamayoifanya huku wakiwasaidia kuhusu sula la masoko.

Naye mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Kigoma  Yassin Mtalikwa aliwataka wajasiliamali hao wa vikundi  fedha wanazozipata wazitumie kwa usahihi  katika shughuli za kiuchumi na  kuzirejesha kwa wakati huku akisisitiza serikali ya awamu ya tano kupitia chama cha mapinduzi  (CCM) imejipambanua katika kuhakikisha inawasaidia makundi hayo kupitia halmashauri zote nchini.

Naye meya wa manispaa hiyo Ndugu. Hussein Ruhava akimkaribisha mgeni rasmi aliwataka wale wanaopokea mikopo hiyo wahakikishe mikopo hiyo inaleta mabadiliko katika shughuli zao za kiuchumi na kufanya uchumi unakua na kusema  halmashauri itaendelea kutoa mikopo kutokana na mapato ya ndani lakini pia baraza la madiwani litasimamia mikopo hiyo inatolewa na kurejeshwa pasipo mgogoro  ya aina yeyote

Naye mgeni rasmi  Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emmanuel Maganga  akihutubia aliipongeza halmashauri kwa utoaji wa mikopo kwa wajasiliamali hao huku akiwataka akina mama kuitumia mikopo hiyo kwa shughuli iliyokusudiwa  ya ukuzaji uchumi wa familia, halmashauri na Taifa kwa ujumla

“ili kuleta tija katika kuwanufaisha wajasiliamali  mikopo hiyo ambayo inatolewa na halmashauri kupitia mapato yake ya ndani ni heri kuwapatia makundi machache ya wajasiliamali fedha kubwa na kuleta matokeo makubwa kuliko kupatia makundi mengi ya wajasiliamali na fedha kidogo” alisema mgeni rasmi huyo

Aliendelea kusema  katika mkoa wa Kigoma omba omba wameongezeka kwa kiasi kikubwa jambo ambalo amelipiga marufuku na kumuagiza  mkuu wa wilaya hiyo ya Kigoma ombaomba atakayeonekana achukuliwe hatua na wale wanaotoa misaada wahakikishe misaada yao wanaipeleka katika vituo vya kulea watu wenye mahitaji maalumu

Alizitaka mamlaka zinazotoa vibali vya kufanya biashara nchi jirani zihakikishe zinatoa vibali haraka ili wajasiliamali wa sabuni, vitenge na mashuka waweze kupeleka nchi za Burundi, Kongo na Rwanda kwa lengo la kupanua wigo wa masoko ya vikundi hivyo vya wajasiliamali.

Akihitimisha hotoba yake aliwataka wakazi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika zoezi zima la uandikishaji linaloendelea katika mkoa huo na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuchagua viongozi waliosahihi na watakaowasaidia katika kukuza uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa