• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI YATOA AJIRA ZAIDI YA 80 KWA WAKAZI WAKE. Employment for resident

Posted on: July 5th, 2019

Halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji jana july 4, imesainisha mikataba ya ajira kwa watoza ushuru na wafanya usafi kwa watu zaidi ya themanini  katika ukumbi wa halmashauri hiyo.

Akiwahutubia waajiriwa hao  Kaimu wa idara ya  Utumishi  Ndugu Iddy  Kalingoji aliwataka katika utumishi wao watakaoufanya  baada ya kujaza mikataba kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kufikia malengo yaliyokusudiwa katika halmashauri hiyo katika ukusanyaji mapato na kuhakikisha mji unakuwa safi kwa wale wafanya usafi.

Aliendelea kusema  mkataba utakaokuwa unajazwa ni wa mwaka mmoja mmoja na kutokufikia malengo kwa ajira uliyopewa ndicho kipimo  cha kujua utendaji kazi wako hali itakayofanya kutoendelea katika ajira hiyo kwa kipindi kingine.

Aliendelea kuwataka kuwa na maadili katika utendaji kazi katika utumishi katika matumizi ya lugha katika utendaji kazi na mwonekano wao katika mavazi yanayofaa ili kuweza kuleta ufanisi katika kazi hizo.

Naye Mwekahazina wa halmashauri hiyo akiwahutubia waajiriwa hao wa Ukusanyaji mapato aliendelea kuwasisitiza kuwa  waaminifu kutokana na masuala ya ukusanyaji wa fedha  baadhi ya watu kushindwa kuwa waamifu.

Aliendelea kusema watasambazwa katika vyanzo mbalimbali vya mapato vilivyopo ikiwa ni pamoja na stendi na masoko yaliyopo ndani ya halmashauri hiyo na vyanzo hivyo tayari vimefanyiwa utafiti wa viwango vyake vya fedha kwa kutumia mawakala na watendaji wa halmashauri hali itakayofanya mkusanyaji kutodanganya katika shughuli hiyo.

Aliendelea kusema ajira hizo walizopata watoza ushuru lengo ni kuleta mapinduzi ya ukusanyaji mapato makubwa ukilinganisha na kipindi cha awali walipokuwa wakitumia watendaji na mawakala katika ukusanyaji huo.

Naye kaimu wa kitengo cha Tehama  Yona Kisusi akizungumza katika ukumbi huo na wakusanya mapato alisema wakusanya mapato hao watapewa mashine za ukusanyaji mapato(POS) ambazo ndizo zitakazotumika kuwapa risti wateja watakao kuwa wanalipa ushuru na tozo zingine.

Aliendelea kusema katika matumizi ya mashine hizo za ukusanyaji mapato (POS) wamekuwepo watu ambao sio waaminifu kwa kujaribu kuibia mapato halmashauri kupitia mashine hizo jambo ambalo ni hatari zaidi na atakayefanya hivo atachukuliwa hatua.

Aliendelea kusema “tayari mbinu zinazotumika katika kuiba mapato ya halmashauri kupitia mashine za kukusanyia mapato tumeshazijua ikiwa na baadhi kutoa ripoti badala ya risti halali, na wengine kuzima data pindi wanapokuwa katika ukusanyaji mapato hakikisha usifanye hivo na uhakikishe unakuwa makini kwa kutumia mashine kwa usahihi  maana kama ukienda kinyume  tutakubaini na kukuchukulia hatua”.

Naye afisa afya wa manispaa Ndugu. Chobaliko akizungumza na wafanya usafi aliwataka kuhakikisha mji unakuwa msafi na unakuwa katika hali ya ushindani na miji mingine huku akiahidi kutoa vifaa vya usafi na kuwasambaza katika maeneo mbalimbali ya usafi katika manispaa hiyo ikiwa ni pamoja na masoko, stendi za halmashauri .

Nao baadhi ya waajiriwa  wakizungumza katika ukumbi huo Ndugu. Bundala Joseph  mtoza ushuru na zubeda Richard  mfanya usafi waliishukuru halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kutoa fursa za ajira hali itakayopunguza vijana wengi kujiingiza katika makundi yasiyofaa kutokana na ukosefu wa ajira.

Picha zaidi ingia   www.kigomaujijimc.go.tz  katika maktaba ya picha.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa