• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HALMASHAURI ZA MKOA WA KIGOMA ZAAGIZWA KUJENGA MABWAWA YA SAMAKI KWA KILA SHULE YA MSINGI NA SEKONDARI. NANE NANE FESTIVAL

Posted on: August 9th, 2019

Mkuu wa mkoa wa kigoma Brigedia Mstaafu Emmanuel Maganga ameagiza kwa shule zote za msingi  na sekondari zilizopo katika mkoa wa Kigoma wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanajenga mabwawa ya samaki kwa ajili ya kitoweo na kujifunza stadi ya maisha.

Ameyasema hayo jana katika kilele cha sikukuu ya wakulima nane nane kanda ya magharibi alipokuwa akihutubia  wananchi katika kufunga maonesho hayo  yaliyofanyika mkoani Tabora eneo la ipuli katika uwanja wa Fatuma Mwasa ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Akihutubia uwanjani hapo aliipongeza serikali ya awamu ya tano kwa jitihada inayofanya katika kuwahudumia wakulima na wafugaji kwa kumaliza migogoro baadhi ya maeneo nchini na kuendelea  kutenga maeneo ili kuondoa migogoro ambayo yaweza kujitokeza.

Aliendelea kusema mkoa wa kigoma kwa mwaka 2016 ulikuwa mkoa wa mwisho kiuchumi kitaifa lakini hadi sasa mkoa umepanda juu kwa nafasi tano kuonesha uchumi wa mkoa wa Kigoma unakuwa kila siku huku akiwakaribisha wawekezaji kujitokeza kwa kiwango kikubwa kuja kuwekeza katika mkoa wa Tabora na kigoma .

Aliendelea kuzitaka halmashauri za kanda ya magharibi kuendelea kukuposha na kutoa elimu kwa makundi ya wanawake, walemavu na vijana kupitia maafisa maendeleo wa jamii waliopo katika halmashauri hizo na kutokaa katika ofisi zao huku makundi hayo yakikiosa elimu ya ujasiliamali.

Aliendelea kusema maafisa ugani bado hawajafanya sehemu yao yao ya kazi ya kuwaelimisha  na  kuwatembelea wakulima na wafugaji katika maeneo yao ya kazi huku akiwataka wananchi kuwakamata maafisa hao pindi wanapokuwa wanatembea mitaani ovyo  na kutoa taarifa katika ofisi ya mkuu wa mkoa huyo

Aliendelea kuzitaka kila  halmashauri  kubaki na maofisa ugani wa tatu ofisini na wengine wote kusambazwa katika vijiji kwa ajili ya kufanya majukumu yao na kuhakikisha uchumi wa familia , mikoa na nchi unakuwa kwa kasi inayotakiwa.

Akiendelea kuhutubia uwanjani hapo aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ulioko mbele yetu na wanawake, wanaume na vijana kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali huku akisisitiza kuchagua viongozi makini watakaoleta tija  na matokeo makubwa kiuchumi ndani ya jamii.

Aliendelea kuzitaka halmashauri za  mkoa wa Kigoma kuhakikisha ifikapo mwezi Septemba zinajenga mabanda yao ya kudumu  ya maonesho ya wakulima katika eneo hilo la Ipuli viwanja vya Fatuma Mwasa na kuacha tabia za kupewa mabanda na halmashauri za mkoa wa Tabora.

Katika kuhititimisha hotuba na Mkuu wa mkoa huyo wa Kigoma aliongeza siku nne za maonesho kwa wakulima na wafugaji kwa lengo la kuendelea kujifunza na kufanya biashara mbalimbali zinazoendelea kufanyika katika eneo hilo.

Naye mkuu wa mkoa wa Tabora Ndugu. Agrey Mwani alimpongeza mkuu wa mkoa huyo wa Kigoma kwa kukubali kuja kuwa mgeni rasmi wa maonesho hayo ya wakulima na kufurahia ukaguzi wa mabanda alioufanya mgeni rasmi huyo na kutoa zawadi kwa halmashauri zilizofanya vizuri .

Mkuu wa mkoa huyo wa Tabora aliendelea kusema serikali ya awamu ya tano inajali masilahi ya wakulima na wafugaji na tayari zimetengwa Bilion mia sita za kuwasambazia maji wananchi wa  mkoa huo  kutoka katika ziwa Victoria.

Mkuu wa mkoa huyo alisisitiza wananchi wa kanda ya magharibi kuendelea kulima mazao ya kimkakati michikichi, pamba na tumbaku na kusema serikali kupitia taasisi za benki zinawakopesha wananchi mitaji ili kuweza kukuza mazao hayo.

Maonesho hayo ya kanda ya magharibi yamenogeshwa kwa nyimbo, maagizo na ngumi za bondia katika kusheherekea sikukuu hiyo huku wajasiliamali wakiendelea kufanya biashara mbalimbali katika eneo hilo la Ipuli katika viwanja vya Fatuma Mwasa.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa